Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Uchaguzi TLS, Dk. Mwakyembe aanza kupukutika
Habari MchanganyikoTangulizi

Uchaguzi TLS, Dk. Mwakyembe aanza kupukutika

Harrison Mwanyembe, Waziri wa Katiba na Sheria Tanzania
Spread the love

WAZIRI wa Sheria na Katiba, Dk. Harrison Mwakyembe, siyo mjumbe wa mkutano mkuu wa uchaguzi wa chama cha wanasheria Tanganyika (TLS) na hivyo hataweza kupiga kura, anaandika Saed Kubenea.

Dk. Mwakyembe ambaye ni wakili wa mahakama kuu, hataruhusiwa kupiga kura kwa kuwa hayumo kwenye orodha ya mawakili walioidhinishwa na Jaji mkuu kwa mwaka huu.

Taarifa zinasema, Dk. Mwakyembe hakuidhinishwa kuwa wakili kutokana na kushindwa kulipa ada zake za kila mwaka kama ilivyoekezwa na sheria za nchi na kanuni za TLS.

Katika siku za hivi karibuni, Dk. Mwakyembe amekuwa akitoa kauli tata kupinga chama hicho kupitisha wagombea anaodai ni wanasiasa na kusema, “hilo likitokea, serikali haitasita kuifuta TLS.”

Dk. Mwakyembe hajamtaja mwana taaluma ambaye ni mwanasiasa na ambaye anataka kugombea urais wa chama hicho.

Hata hivyo, anayeonekana kulengwa na Dk . Mwakyembe, ni Tundu Lissu, wakili machachari nchini, mbunge wa Singida Mashariki na mwanasheria mkuu wa Chama cha Demokrsia na Maendeleo ( Chadema).

Lissu, ni miongoni mwa wagombea wanne wa wanafasi ya Rais wa TLS.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Equity Bank yaendelea kusotea mabilioni ya fedha mahakama rufani

Spread the loveBENKI za Equity ya Tanzania na Kenya, zimeendelea kupambana mahakamani...

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

error: Content is protected !!