Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa ‘Katiba pendekezwa itachochea Wazanzibar kudai uhuru’
Habari za Siasa

‘Katiba pendekezwa itachochea Wazanzibar kudai uhuru’

Othamn Masoud Othman, aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar
Spread the love

OTHMAN Masoud Othman, aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar kabla ya kutimuliwa kwa kuunga mkono mapendekezo ya serikali tatu, amesema Katiba inayopendekezwa  itajenga mfumo utakaosababisha kizazi kijacho cha Zanzibar kidai uhuru badala ya haki ndani ya Muungano, anaandika Pendo Omary.

Othman alifutwa kazi na Dk. Ali Mohamed Shein, Rais wa Zanzibar na nafasi yake kuchukuliwa na Said Hassan Said baada ya kumalizika kwa Bunge Maalum la Katiba 2014, ambapo alipiga kura ya wazi ya kuunga mkono mapendekezo ya serikali tatu kinyume na msimamo wa chama tawala.

Akizungumza katika mkutano wa kwanza wa kitaifa wa Katiba uliofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita jijini Dar es Salaam na kuandaliwa na Jukwaa la Katiba Tanzania (Jukata), Othman amesema;

“Kwa ujumla Katiba inayopendekezwa sio tu kwamba imerasimisha kero za Muungano lakini inajenga mfumo utakaofanya kizazi kijacho cha Zanzibar kidai uhuru badala ya haki ndani ya Muungano.”

Amesema katika kujenga mustakbali wa kikatiba ndani ya Tanzania, suala la Muungano haliwezi kuepukwa kuwa ajenda kubwa na ya msingi.

“Taifa letu limepata uzoefu wa kutosha wa kasoro za Muungano.  Ni dhahiri kuwa itikadi na kutokuwepo upeo na uthabiti katika kujenga mfumo mpya wa kikatiba kumesababisha Katiba inayopendekezwa kuwa mbaya na dhaifu zaidi, katika kujenga mustakbali huo,” amesema Othman.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!