Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Mbunge awakingia kifua wavamizi
Habari Mchanganyiko

Mbunge awakingia kifua wavamizi

Msitu wa Minyugye ulioppo wilaya ya Ikungi. Picha ndogo ni Elibariki Kingu, Mbunge wa Jimbo la Singida Magharibi
Spread the love

ELIBARIKI Kingu, Mbunge wa Jimbo la Singida Magharibi anatuhumiwa kuchochea kuongezeka kwa vitendo vya uvamizi katika msitu wa hifadhi wa Minyughe, wilayani Ikungi, anaandika Mwandishi wetu.

Mbunge huyo anadaiwa kuwalipia faini wananchi ambao wamekuwa wakikamatwa, kushtakiwa na kuhukumiwa mahakamani kwa makosa ya uvamizi wa msitu huo. Anadaiwa kutumia nafasi hiyo kama jukwaa la kisiasa la kumuongezea ushawishi kwa wananchi.

Taarifa hizi zinakuja wakati ripoti zikiwa zinaonesha kuwa zaidi ya wakazi 41 wa kijiji cha Mtavira, kata ya Makilawa, Wilaya ya Ikungi, mkoani Singida wamefikishwa katika Mahakama ya Mwanzo ya Ikungi kwa tuhuma za kuvamia msitu wa hifadhi ya Minyughe.

Michael Lyimo, Kaimu Meneja wa Wakala wa Misitu Tanzania (TFS) amesema, “Tuafanya juhudi kubwa lakini bado matokeo siyo mazuri sana kwani wananchi waliohukumiwa kwa uvamizi wanalipiwa adhabu ya faini na Mbunge wao. Kama wangelipa wenyewe wangeona umuhimu wa kutovamia msitu wa hifadhi.”

Lyimo amedai kuwa wanasiasa wamekuwa wakiutumia msitu huo kujipatia umaarufu wa kisiasa na kusaka kura kwa kuwashawishi wananchi kuwa waendelee kuishi ndani ya msitu huku wanasiasa wengine wakiahidi kuufanya msitu huo wa hifadhi kuwa eneo la makazi iwapo watachaguliwa.

Mpaka sasa, jumla ya kaya 76 zilizokuwa zikiishi katika nyumba zilizokuwa ndani ya hifadhi zimehamishwa kwa nguvu na nyumba hizo kuvunjwa.

“Nawasihi wanasiasa watafute namna nyingine ya kuomba kura na kutafuta umaarufu wa kisiasa kwasababu uhifadhi wa mazingira una faida nyingi hata kwa kizazi kijacho, hivyo historia itakuja kuwahukumu waharibifu wa mazingira,” amefafanua Lyimo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Makonda autaka mgodi kubadilisha maisha ya wana-Geita

Spread the loveMKUU wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda ametoa wito kwa...

Habari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Je, miji ya Uingereza inafilisika?

Spread the loveMNAMO 1890, mwandishi mmoja wa habari Mmarekani aitwaye Julian Ralph...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Equity Bank yaendelea kusotea mabilioni ya fedha mahakama rufani

Spread the loveBENKI za Equity ya Tanzania na Kenya, zimeendelea kupambana mahakamani...

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

error: Content is protected !!