Sunday , 28 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Wastaafu waililia Serikali ya JPM
Habari Mchanganyiko

Wastaafu waililia Serikali ya JPM

Spread the love

ZAIDI ya wastaafu 300 kutoka wilaya za Nyamagana na Ilemela Mkoani Mwanza, wameilalamikia Serikali kwa kuwakata makato makubwa ya pensheni zao za kila miezi mitatu kwani hayaendani na hali halisi ya maisha, anaandika Moses Mseti.

Wakizungumza leo katika zoezi la kufanyiwa uhakiki, linalofanywa na Wizara ya Fedha na Mipango wamedai kwamba licha ya makato hayo makubwa bado pensheni wanayolipwa kwa mwezi haizidi Sh. 80,000/= na 90,000/=

“Kiasi cha fedha tunacholipwa, hakiendani na hali ya maisha ya sasa. Serikali inapaswa kuangalia namna bora ya kutuongezea pensheni za kila mwezi au baada ya miezi mitatu ili kuendana na hali halisi ya maisha,” amesema Salome Sabula, mmoja kati ya wastaafu hao.

Kwa upande wake mstaafu mwingine aliyejitambulisha kwa jina la Elizabeth Sylvester amesema, “mimi watoto wangu nimesomesha lakini mpaka sasa baada ya Serikali kusitisha ajira wapo tu nyumbai bado naendelea kuwasomesha wengine, sasa Sh. 80, 000/= tunazolipwa kwa mwezi zitasaidia nini?”

Wamesema kipindi walipostaafu mwaka 1990, walilipwa Sh. milioni 4.4 tu huku walimuomba Rais John Magufuli, kuwaangalia wastaafu wa zamani ili waongezewe fedha ili kukabiliana na makali ya maisha.

Stanslaus Mpembe, Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali, Wizara ya Fedha na Mipango amesema lengo la uhakiki wa wastaafu wanaolipwa na wizara hiyo kwenye mikoa mitano ya Kanda ya ziwa unalenga kubaini wastaafu sahihi wanaopaswa kulipwa na serikali.

“Pamoja na kuhakiki wastaafu hao pia tunalenga kuondoa malalamiko na changamoto za wastaafu zilizokuwepo kwa muda mrefu na tunawahimiza wajitokeza kuhakikiwa kabla ya zoezi hilo kukamilika mnamo tarehe 13 Januari mwaka huu,” amesema Mpembe.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NBC yapata tuzo ya mwezeshaji bora wa mikopo serikali Afrika

Spread the loveBenki ya NBC imepata tuzo ya Mwezeshaji Bora wa Pamoja...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Biteko aipongeza GGML kudhibiti vifo, majeruhi mahali pa kazi

Spread the loveNAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari Mchanganyiko

Wami Ruvu hawana deni la Rais Samia katika kutunza vyanzo vya maji

Spread the love  BODI ya Maji Bonde la Wami Ruvu, imeendelea kuchua...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

error: Content is protected !!