Monday , 5 June 2023
Home Kitengo Michezo FIFA waongeza idadi ya timu Kombe la Dunia
Michezo

FIFA waongeza idadi ya timu Kombe la Dunia

Gianni Infantino, Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani (Fifa)
Spread the love

SHIRIKISHO  la Mpira wa Miguu Dunia (Fifa) kupitia wajumbe wake, wamefikia makubaliano ya  kuongeza idadi za timu kufikia 48 kutoka 32 zilizokuwa zikishiriki Kombe la Dunia hapo awali, na utaratibu huo utaanza kutumika katika fainali za mwaka 2026.

Fifa wamefikia hatua hiyo baada ya kupiga kura katika mkutano mkuu wa uliofanyika Zurich ambapo kwa sasa timu 48, zitakuwa katika makundi 16 na kila kundi litakuwa na timu tatu na sio nne kama ilivyokuwa hapo awali.

Timu mbili za juu zitafuzu katika hatua ya 32 bora na idadi ya mechi zitaongezeka kufikia 80 badala ya 64 na michuano hiyo itachezwa kwa siku 32.

Lengo la kuongeza idadi ya timu katika michuani hiyo ni kufanya mchezo wa mpira kuendelea duniani kote na kuongeza washiriki kutoka mabara ambayo yalikuwa na idadi ndogo ya timu katika kombe hilo.

Hii ni mara ya pili kwa FIFA kuongeza idadi ya timu shiriki katika michuano hiyo baada ya mwaka 1998, katika fainali zilizofanyika Ufaransa ushiriki wa timu uliongezeka kutoka 24 mpaka 32 ambazo zitafikia kikomo 2022 katika fainali zitakazofanyika Quatar kabla ya kuanza kwa utaratibu mpya 2026.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Samia aipongeza klabu ya Yanga kwa hatua iliyofikia

Spread the love RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia...

Michezo

Yanga waitwa Ikulu kesho Jumatatu

Spread the love RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, kesho Jumatatu, tarehe...

Michezo

Dk. Mkwizu: Afrika tudumishe utamaduni

Spread the love  MWENYEKITI wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Mkoa wa...

Michezo

‘EONII’ kuteka tasnia ya filamu

Spread the love  UZINDUZI wa Filamu ya Kisayansi ya ‘EONII’ uliofanyika Mei...

error: Content is protected !!