Saturday , 2 December 2023
Home Gazeti Habari za Siasa 169 udiwani CCM wapeta Kilimanjaro
Habari za Siasa

169 udiwani CCM wapeta Kilimanjaro

Spread the love

WAGOMBEA udiwani 169 kati ya 1145 ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), walioomba kuteuliwa kugombea udiwani kupitia chama hicho mkoani Kilimanjaro, wamepitishwa. Anaripoti Mwandishi Wetu, Moshi … (endelea).

Majina ya madiwani hao yametangaza rasmi jana tarehe 17 Agosti 2020 na Katibu wa CCM Mkoa wa Kilimanjaro, Jonathan Mabihya wakati akizungumza na vyombo vya habari mkoani humo baada ya kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa.

”Wagombea hawa 169 ndio waliopendekezwa na kuteuliwa na kikao cha Halmashauri Kuu kwa ajili ya kupeperusha bendera ya CCM kwenye uchaguzi Mkuu wa mwaka huu,” amesema na kuongeza:

”Ni dhahiri kuwa, mchakato wetu wa kikatiba na kikanuni uliendelea baada ya kura za maoni kupigwa. Vikao vya uchujaji  na utoaji mapendekezo viliendelea ambapo kamati zote za siasa kuanzia kata hadi mkoa zilikaa na kutoa maoni na mapendekezo yake.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia kuzindua programu ya nishati safi ya kupikia kwa wanawake Afrika

Spread the loveRais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuzindua programu ya...

Habari za Siasa

AG aiagiza kamati ya maadili kuwashughulikia mawakili wanaokiuka maadili

Spread the loveMWANASHERIA Mkuu wa Serikali (AG), Dk. Eliezer Feleshi, ameagiza Kamati...

Habari za Siasa

Jaji avunja ukimya sakata la Mpoki kusimamishwa uwakili

Spread the loveJAJI Mkuu wa Tanzania, Prof. Ibrahim Juma, amekitaka Chama cha...

Habari za Siasa

Sheikh Ponda ataka mwarobaini changamoto uchaguzi 2020

Spread the loveKATIBU Mkuu wa Shura ya Maimamu Tanzania, Sheikh Ponda Issa...

error: Content is protected !!