Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lema: Nimechuku fomu niendelee kuwa mbunge
Habari za Siasa

Lema: Nimechuku fomu niendelee kuwa mbunge

Spread the love

GODBLESS Lema, amechukua fomu ya kuwania Ubunge Arusha Mjini kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu, Arusha…(endelea)

Lema amefika Ofisi ya Mkurugenzi wa Jiji la Arusha leo Jumanne tarehe 18 Agosti 2020 akiwa anaendesha gari yeye mwenyewe pamoja na familia yake akiwemo, Neema Tarimo.

Lema ambaye ameongoza jimbo hilo kwa miaka kumi mfululizo, amekabidhiwa fomu na Msimamizi wa Uchaguzi wilaya ya Arusha, Dk John Pima.

Baada ya kukabidhiwa, Lema amezungumza na waandishi wa habari akisema ana uhakika wa kuibuka tena mshindi katika uchaguzi huo kwa sababu wananchi wanamtaka mbunge anayezungumzia masuala yao badala ya kuisifia Serikali.

Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema

“Nimekuja kuchukua fomu ili niendelee kuwa mbunge wa jimbo la Arusha Mjini, nimeona majina ya wanaotaka kugombea ubunge jimbo hili, hawaninyimi usingizi,” amesema Lema

Amesema, mwaka 2015 “Chadema tulishinda Kata 24 udiwani moja ikaenda CCM, lakini sasa tumeshaweka mikakati ya kuchukua Kata zote.”

Amesema wapigakura wamekua na mashaka ya kura kuchakachuliwa na kuonya uchaguzi mkuu haupaswi kuchezewa kwasababu unaweza kusababisha uvunjifu wa amani na hawatakua tayari kuibiwa kura.

Lema amesema hata kitendo cha kuchomwa ofisi yao ya kanda ni dalili za uvunjifu wa amani na wameshamkabidhi kamanda wa Polisi mkoa majina ya waliotekeleza kitendo hicho ambao watawataja hivi karibuni.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!