Watu 25 wamefariki dunia papo hapo mkoani Arusha katika ajali ya barabarani iliyohusisha magari matatu. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha SACP Justine Masejo, kati ya watu hao watatu ni wa familia moja ya Abdulrazak Mohamed maarufu ‘Chucha’ wa Ngaramtoni.
Akizungumzia na waandishi wa habari Kamanda Masejo amesema ajali hiyo imetokea leo tarene 24 Februari majira ya saa 11 jioni baada ya lori lililokuwa likitokea Namanga kuelekea Arusha kuyagonga magari matatu.
Bila kutaja jina la dereva aliyekuwa akiendesha lori hilo, Kamanda Masejo amesema taarifa za awali zinaonyesha Lori lilipoteza uelekeo hali iliyopelekea kuyagonga magari hayo.
Amesema majeruhi wa ajali hiyo wapo katika hali mbaya na wanaendelea na matibabu.
Hata hivyo, amewaomba wananchi ambao ndugu zao walikuwa wakisafiri kupitia barabara hiyo kufika katika hospitali ya Mkoa wa Arusha Mount Meru kwa ajili ya utambuzi wa marehemu pamoja na majeruhi ambao wanatibiwa hapo.
Leave a comment