Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Zitto kusuka, kunyoa Febr 10 
Habari za Siasa

Zitto kusuka, kunyoa Febr 10 

Spread the love

UAMUZI wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam kuhusu kesi ya uchochezi namba 327/2018 inayomkabili Zitto Kabwe, kwamba ana kesi ya kujibu ama la! utajulikana tarehe 10 Februali 2020. Anaripoti Faki Sosi, Dar es Salaam … (endelea).

Upande wa Jamhuri umewasilisha mashahidi 15 mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi ambapo tayari umefunga pazia la ushahidi wao. Kwa sasa Hakimu Huruma yupo likizo.

Leo tarehe 10 Januari 2020, mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Vicky Mwaikambo, wakili wa serikali mkuu Tumain Kweka, ameiambia mahakama, upande huo umemaliza kutoa ushahidi wao na wamewasilisha hoja za kuitaka mahakama kwa ushahidi huo ione kuwa Zitto, Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo anakesi ya kujibu.

Wakili wa utetezi Bonifacia Mapunda, ameieleza mahakama kuwa wamejibu hoja hizo na kwamba, hawaoni sababu ya kuongeza hoja (Rejoinder).

Hakimu Mwaikombo amesema, mahakama itatoa uamuzi tarehe 10 Februari mwaka 2020. Zitto anakabiliwa na mashtaka matatu ya uchochezi anayodaiwa kuyatenda tarehe 38 Oktoba 2018.

Anadaiwa kutenda makossa hayo katika mkutano wake na waandishi wa habari, uliofanyika katika ofisi za makao makuu ya chama hicho, Kijitonyama jijini Dar es Salaam.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!