Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Tunakwenda kuitawala Dodoma – Chadema
Habari za Siasa

Tunakwenda kuitawala Dodoma – Chadema

Jiji la Dodoma
Spread the love

CHAMA Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Kanda ya Kati kimeeleza dhamira yake ya kuongoza Jiji la Dodoma. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Lazaro Nyalandu, Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Kati amesema, desturi ya Chadema ni kuhakikisha inaondoka sehemu ambayo viongozi wengi wa serikali walipo.

“Tutatumia mbinu zinazojulikana na zisizojulikana kuhakikisha CCM Kanda ya Kati inafutika. CCM waanze kuona ni namna gani ya kujipanga kwa muda wa miaka mitano wakiwa wapinzani na Chadema kikiwa chama tawala,” amesema.

Hata hivyo amesema, Serikali ya Awamu ya Tano ambayo yeye ameitumikia, imetawaliwa na woga amesisitiza umuhimu wa vyama vya siasa kuwa huru kufanya siasa kwa maslahi ya umma.

Nyalandu amesema, njia ya uhuru katika demokrasia ni kuwa na Tume Huru ya Uchaguzi isiyoamuliwa na mteuzi wa watendaji wa tume hiyo.

“Wakati nikiwa CCM, Singisa tulikuwa na kata moja ya uchaguzi mdogo, lakini ilikuwa ngumu na wakati huo rais wangu Kikwete (Rais Jakaya Kikwete) alinipigia simu akanieleza, kniende kuongeza nguvu.

“Wapo waliotuelewa na wengine hawakutuelewa, baada ya kupiga kura CCM tulitandikwa mbali sana, nilimpigia Rais Kikwete nikamueleza kuwa tumepigwa mbali sana, naye akasema basi kubalina na matokeo, hiyo ndio siasa tunayoitaka,” amesema Nyalandu.

Pia amesema, licha ya vyombo vya dola kufanya vizuri katika kulinda usalama wa mipaka, usalama wa raia na mali zake, lakini wafanye kazi zao kwa ueledi na kuheshimu viapo vyao.

Amesema, vyombo vya usalama visijiingizwe katika siasa na wala wasifanye kazi za siasa, kwani kazi za siasa ni za wana siasa na si vinginevyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!