Wednesday , 8 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa TLS yajitosa kumtetea Fatma Karume
Habari za Siasa

TLS yajitosa kumtetea Fatma Karume

Fatma Karume
Spread the love

CHAMA cha Wanasheria Tanganyika (TLS) kimejitosa kumtetea Fatma Amani Karume aliyehukumiwa na kamati ya Maadili ya Mawakili kuondolewa jina lake (namba 848) kwenye orodha ya mawakili wa TLS. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea). 

Uamuzi huo ulitolewa tarehe 23 Oktoba 2020 ikiwa imepita mwaka mmoja tangu Mahakama Kuu ya Tanzania kumsimamisha uwakili ikimtuhumu kutoa matamshi yaliyolalamikiwa na Serikali.

Tarehe 20 Septemba 2019, Mahakama Kuu ya Tanzania ilitoa uamuzi huo wa kumsimamisha na kupeleka suala hilo, Kamati ya Maadili ya Mawakili Tanganyika kwa hatua zaidi.

Fatma ambaye amewahi kuwa Rais wa TLS kati ya mwkaa 2018/19 alikutwa na tuhuma hizo alipokuwa akimtetea aliyekuwa Katibu Mwenezi wa ACT-Wazalendo, Ado Shaibu katika kesi aliyoifungua mahakamani hapo kupinga uteuzi wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Profesa Adelardus Kilangi.

Dk. Rugemeleza Nshala, Rais wa TLS

Fatma, ambaye ni ni mtoto wa Rais mstaafu wa Zanzibar, Aman Abei Karume alilalamikiwa na upande wa Serikali katika kesi hiyo juu ya matamshi yake. Uamuzi huo ulitolewa na Jaji Kiongozi wa Tanzania, Dk. Eliezer Feleshi ambaye pia aliiondoa kesi hiyo.

Jana Jumanne, Rais wa TLS, Dk. RUgemeleza Nshala alitoa taarifa ya jinsi watakavyojitosa kumtetea Fatma pindi atakapokara rufaa kupinga uamuzi huo.

Soma taarifa yote ya Dk. Nshala hii hapa chini

;

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia: Matumizi ya nishati safi sio anasa, ladha ipo

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amesema matumizi ya nishati safi kwa...

Habari za SiasaTangulizi

Samia: Kuanzia Agosti marufuku kutumia mkaa, kuni

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amemuagiza Waziri wa Nchi, Ofisi ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mwendokasi Kigogo – Segerea kujengwa awamu ya 5

Spread the loveNaibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (TAMISEMI), Festo Dugange...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Rais Samia ni Mzanzibari: Shida Iko Wapi?

Spread the loveTAIFA linakabiliwa na upungufu wa fikra sahihi. Upungufu huu unaonekana...

error: Content is protected !!