Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli amfariji Zitto
Habari za SiasaTangulizi

Rais Magufuli amfariji Zitto

Zitto Kabwe, Kiongozi Mkuu wa ACT-Wazalendo
Spread the love

RAIS John Magufuli amempa pole Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe aliyepata ajali ya gari jana tarehe 6 Oktoba 2020. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Zitto alipata ajali akiwa njiani kuekelea kwenye mkutano wa kampeni kweye Jimbo la Kigoma Kusini akitokea Kata ya Kalya Lukoma mkoani Kigoma.

Kwa mujibu wa Gerson Msigwa, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais-Ikulu, Rais Magufuli amempigia simu Zitto na kumpa pole.

Rais John Magufuli

“Rais Magufuli amempigia simu na kumpa pole Zitto Zuberi Kabwe aliyepata ajali ya gari jana Mkoani Kigoma. Amemuombea heri ili apone haraka na pia amewashukuru Madaktari na Wauguzi wa Kituo cha Afya cha Kalya na Hospitali ya Maweni kwa matibabu waliyompa,” ameandika Msigwa kwenye ukurasa wake wa Twitter.

Katika ajali hiyo  Zitto alikuwa na watu watatu katika gari yake ambao wote walijeruhiwa. Na kukimbizwa katika Kituo cha Afya cha Kalya wilayani Uvinza mkoani Kigoma.

Mapema leo Zitto pamoja na majeruhi wengine wamewasili jijini Dar es Salaam kwa ajili ya matibabu zaidi.

Kupitia ukurasa wake wa Twitter, Zitto amesema ilikuwa ajali mbali ila kwa Neema za Mungu ametoka salama.

‘Ninaendelea vizuri. Ilikuwa ajali mbaya sana. Namshukuru Allah kwa kutuponya. Shukran Wahudumu wa Kituo cha Afya Kalya, licha ya changamoto, Huduma ya kwanza imetusaidia. Shukran Madaktari na Wahudumu Hospitali ya Maweni Kigoma. Mimi na wenzangu, mpaka sasa, ni wazima,” ameandika Zitto.

Baada ya Zitto kuandika ujumbe huo,wanasiasa mbalimbali wamempa pole, akiwemo Nape Nnauye, aliyekuwa Munge wa Mtama kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM),  January Makamba, Mbunge wa Bumbuli, Ummy Mwalimu, Waziri wa Afya.

“Pole sana kaka Mungu akuponye,” ameandika Nape katika ukurasa wa Twitter wa Zitto.\

John Heche, Mbunge wa Tarime Vijiji aliyemaliza muda wake ameandika “Pole sana kaka, tunamshukuru Mungu kwa kukunusuru na mabaya yote. Tunakutakia uponyaji wa haraka.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!