Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Sheria ya PSSSF yaanza kufanya kazi kesho
Habari Mchanganyiko

Sheria ya PSSSF yaanza kufanya kazi kesho

Spread the love

SHERIA ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumsihi wa Umma (PSSSF) namba 2 ya mwaka 2018 kuanza kutumika rasmi kesho baada ya Waziri wa nchi ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama kuitangaza rasmi. Anaripoti Dany Tibason … (endelea).

Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumshi wa Umma (PSSSF) ni muunganiko wa mifuko minne ambayo ni PSPF, PPF, LAPF na GEPF.

Wakati sheria ikianza kutumika Mhagama ametangaza majina nane ya wajumbe wa bodi ya PSSSF ambao wameteuliwa kutokana na muundo wa sheria ya kuanzishwa kwa mfuko huo.

Sheria ya PSSSF imetangazwa kuanza rasmi kutumika baada ya bunge kupisha sheria hiyo Januari 31 na Rais John Magufuli kusaini sheria hiyo tarehe 8 Februari, mwaka huu.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini hapa leo Waziri Mhagama amesema kuwa kuanzia sasa Watumishi wa umma watakaoajiriwa watasajiliwa katika mfuko huo na wale watakaoajiriwa katika sekta binafsi watasajiliwa katika mfuko wa NSSF.

Amesema kuwa wanachama wote ikiwa ni pamoja na wastaafu na warithi waliopo katika mifuko iliyounganishwa watahamishiwa katika mfuko wa PSSSF na haki na satahili zao zitaendelea kutolewa na mfuko huo bila kuathiriwa kwa namna yeyote ile.

“Vivyo hivyo rasilimali vitega uchumi, madeni, mifuko ya hiari na mikataba iliyokuwa chini ya mfuko iliyounganishwa itahamishiwa katika mfuko mpya wa PSSSF, hali kadhalika watumishi wote wa mifuko hiyo watahamishiwa katika mfuko mpya ambapo Uongozi wa mfuko huo utawapangia majukumu yao kwa kuzingatia muundo wa mfuko huo,” amesema
Mhagama.

Mhagama amesema kuwa bila kuathiri huduma kwa wanachama kwa namna yeyote ile serikali ilifanya mambo ya kutambua wanachama wastaafu na Wanufaika wote wa mifuko iliyounganishwa sambamba na haki na stahili zao katika mifuko hiyo.

“Kwa kuzingatia maandalizi hayo na jitihada nyingine mbalimbali zilizofanywa na serikali napenda kuwahakikishia na kuwaondoa wasiwasi wanachama wa mifuko iliyounganishwa, wadau wote wa sekta ya hifadhi ya jamii na wananchi wa ujumla kwamba serikali imelifanyia kazi jambo hili kwa umakini mkubwa ili kuhakikisha kwamba zoezi la kuunganishwa
mifuko halitakiwa na athari yeyote kwa uendelevu wa huduma kwa wanachama,” amesema Mhagama.

Wajumbe walioteuliwa kwa mujibu wa sheria ya kuanzishwa kwa mfuko huo ni kutoka katika chama cha wafanyakazi chenye wanachama wengi kwenye mfuko wa PSSSF walioteuliwa ni Leah Ulaya na Rashid Mtima.

Wawakilishi wa waajiri kutoka chama cha waajiri wenye uwakilishi mkubwa ni Dk. Agrey Mlimuka na Stella Katende, mwakilishi kutoka sekta binafsi aliyeteuliwa ni Thomas Manjati ambapo mwakilishi kutoka Tamisemi ni Hanry Katabwa.

Mwakilishi kutoka Wizara ya Fedha na mipango ni Suzan Kabogo, mwakilishi wa wizara yenye dhamana (Owm- KVAU), ni Jacob Mwinuka na nafasi ya mjumbe mmoja kutoka ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali itatangazwa baadaye baada ya utaratibu kukamilika.

Naye Mkurugenzi kuu wa Mfuko wa PSSSF, Eliud Sanga amesema kuwa Mfuko huo umejipanga vizuri kwa ajili ya kuondoa kero za wanachama pamoja na kumaliza usumbufu kwa wanachama wa kucheleweshewa mafao yao.

Naye Mkurugenzi mkuu wa NSSF, William Erio amesema kuwa mifuko hiyo ya hifadhi za jamii imejipanga kutoa huduma bora zaidi kwa wanachama wake ikiwa ni pamoja na kutoa mafao yao kwa wakati kwa mujibu wa sheria mpya.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!