MWENYEKITI wa Chadema Taifa, Freeman Mbowe amepewa onyo na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa kosa la kutohudhuria mahakamani hapo kwa mara mbili. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).
Onyo hilo limetolewa leo tarehe 31 Julai, 2018 na Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri wakati kesi inayomkabili Mbowe na wenzake ilipokuja kwa ajili ya kuwasomea washitakiwa maelezo ya awali.
Hakimu Mashauri amesema iwapo Mbowe atarudia tena kutofika mahakamani kwa sababu zisizo na msingi, dhamana yake itafutwa.
Mbowe ametakiwa na mahakama kuheshimu masharti ya dhamana na kwamba asipofanya hivyo mahakama itamfutia dhamana yake sambamba na kutaifisha fungu la dhamana ambalo ameliweka.
Katika kesi hiyo, Mbowe na wenzake akiwemo Mbunge wa Tarime Mjini, Ester Matiko, Peter Msigwa (Iringa Mjini) na Katibu wa Chadema, Dkt. Vicent Mashinji wanakabiliwa na mashitaka 13 ikiwemo kula njama, kufanya mkusanyiko wenye ghasia, kuhamasisha hisia za chuki pamoja na kushawishi hali ya kutoridhika.
Leave a comment