Thursday , 18 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mahakama yamuonya Mbowe kwa utoro
Habari za Siasa

Mahakama yamuonya Mbowe kwa utoro

Spread the love

MWENYEKITI wa Chadema Taifa, Freeman Mbowe amepewa onyo na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa kosa la kutohudhuria mahakamani hapo kwa mara mbili. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Onyo hilo limetolewa leo tarehe 31 Julai, 2018 na Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri wakati kesi inayomkabili Mbowe na wenzake ilipokuja kwa ajili ya kuwasomea washitakiwa maelezo ya awali.

Hakimu Mashauri amesema iwapo Mbowe atarudia tena kutofika mahakamani kwa sababu zisizo na msingi, dhamana yake itafutwa.

Mbowe ametakiwa na mahakama kuheshimu masharti ya dhamana na kwamba asipofanya hivyo mahakama itamfutia dhamana yake sambamba na kutaifisha fungu la dhamana ambalo ameliweka.

Katika kesi hiyo, Mbowe na wenzake akiwemo Mbunge wa Tarime Mjini, Ester Matiko, Peter Msigwa (Iringa Mjini) na Katibu wa Chadema, Dkt. Vicent Mashinji wanakabiliwa na mashitaka 13 ikiwemo kula njama, kufanya mkusanyiko wenye ghasia, kuhamasisha hisia za chuki pamoja na kushawishi hali ya kutoridhika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Regina Mkonde: CCM yamkana mwenyekiti UVCCM aliyetaka wapinzani wapotezwe

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimejitenga na kauli ya mwenyekiti...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia kutunukiwa udaktari wa heshima Uturuki

Spread the loveBaraza la Chuo Kikuu cha Ankara, ambacho ni cha pili...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia atua Uturuki kwa ziara ya siku 5

Spread the loveRais Samia Suluhu Hassan leo Jumatano amewasili nchini Uturuki kwa...

Habari za SiasaTangulizi

Samia arejesha mikopo ya 10%, bilioni 227.96 zatengwa

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amerejesha utaratibu wa utoaji mikopo...

error: Content is protected !!