Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Zitto amgomea Kangi Lugola
Habari za SiasaTangulizi

Zitto amgomea Kangi Lugola

Spread the love

ZITTO Kabwe, Mbunge wa Kigoma Mjini amegomea wito uliotolewa na Kangi Lugola, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Waziri wa kujisalimisha kwa Mkuu wa Polisi Mkoa wa Lindi ndani ya siku mbili kuanzia sasa. Anaripoti Faki Sosi na Regina Kelvin … (endelea).

Katika ukurasa ukurasa wake wa Twitter Zitto ameandika kuwa, hatokwenda kujisalimisha polisi kama alivyoagiza Lugola.

Kabla ya kauli ya Zitto kutoa kauli hiyo, Waziri Lugola wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo alimtaka kujisalimisha kwa Mkuu wa Polisi Mkoa wa Lindi kwa madai ya kufanya uchochezi.

Lugola alidai kuwa, Zitto alitoa kauli za uchochezi kwenye mkutano wa hadhara alioufanya jana Julai 30 katika viwanja vya Mkapa Garden, Kilwa Masoko mkoani Lindi.

“Baadhi ya Watanzania wenzetu bado wanajihusisha na mambo ya kutoa kauli za uchochezi, kutukana viongozi, kukaidi agizo la rais hasa wabunge kutoka maeneo ya majimbo yao na kwenda kufanya mikutano kwenye majimbo yasiyo ya kwao,” amesema na kuongeza;

“…Wakifika kwenye majimbo yasiyo ya kwao wanajihusisha na kutukana viongozi na kutoa lugha za uchochezi.

“Nimekwisha kemea jambo hili na nimesema chaguzi zote zinazoendelea hivi karibuni na zitakazoendelea mwakani na milele na milele nimesema hakuna atakayepona kama ataendelea kutokana viongozi na kutoa lugha za uchochezi,” amesema.

Amesema, juzi (Julai 29) katika Jimbo la Saidi Bungara Zitto alikaidi agizo hilo na kwenda kufanya mikutano katika jimbo lisilo la kwake.

“Zitto mahali popote alipo ajisalimishe kwa Mkuu wa Polisi Mkoa wa Lindi na endapo asipojisalimisha ndani ya siku mbili, nitamulekeza IGP ili popote alipo akamatwe,” amesema Lugola.

Kutokana na kauli ya Lugola, Zitto ambaye ni Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo amesema waziri huyo hana mamlaka ya kumwagiza ajisalimishe polisi.

Zitto amesema, hatotii wito huo kwa kuwa ni kinyume cha sheria na kwamba, zipo taratibu za Jeshi la Polisi kinyume na zinazotumiwa na Lugola.

Kwenye ukurasa wake ameandika “Waziri hana hayo mamlaka. Kama polisi wananitaka watoe wito wa kisheria nitakwenda. Naendelea na kampeni za Mbunge wa Buyungu ambapo tunamwunga Mgombea wa Chadema na madiwani wa ACTwazalendo kwenye kata kadhaa. Nashauri Waziri ampate kwanza yule Mbwa
wa Polisi Bandari ”

Hata hivyo, Lugola Lugola amemuagiza Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Simon Sirro kumchukulia hatua Mkuu wa Polisi Wilayani Kilwa(OCD) kwa kumruhusu Zitto kuendelea kufanya mkutano katika jimbo lisilo lake.

“ Na pia namulekeza IGP achukue hatua kwa mkuu wa polisi wa wilaya ya kilwa ocd, ya kwa nini hakuchukua hatua dhidi ya zitto kwa kuendelea kufanya yale tuliyoyakataza,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

error: Content is protected !!