KIONGOZI wa upinzani nchini Kenya Raila Odinga ametangaza kuwa hayuko tayari kushiriki marudio ya uchaguzi mkuu wa urais nchini humo.abla ya kufanyika uchaguzi, anaandika Mwandishi wetu.
Odinga amesema kuwa anataka kuwepo mikakati ya kisheria na kikatiba inayohitajika, kabla ya yeye kukubali kushiriki uchaguzi huo.
Amesema anataka Tume ya Uchaguzi na Mipaka ya Kenya (IEBC), kufanyiwa marekebisho kabla ya uchaguzi nchini humo.
Jana Jumatatu Tume ya Taifa ya uchaguzi nchini Kenya ilitangaza kwamba uchaguzi mpya wa urais nchini humo utafanyika tarehe 17 Oktoba.
Mwenyekiti wa tume hiyo, Wafula Chebukati alisema uchaguzi huo utashirikisha wagombea wawili pekee wa urais, Rais Uhuru Kenyatta na Waziri Mkuu mstaafu Raila Odinga.
“Hakutakuwa na uteuzi mpya wa wagombea wa urais katika uchaguzi huo upya. waliopinga matokeo ya uchaguzi kortini, Raila Odinga na mgombea mwenza wake Stephen Kalonzo Musyoka na mshtakiwa wa tatu Rais Uhuru Kenyatta na mgombea mwenza wake, William Samoei Ruto, watakuwa ndiyo wagombea pekee,” alisema
Leave a comment