Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Nape, Dk. Bashiru waungana kukemea wanasiasa kushughulikiwa na Polisi
Habari za Siasa

Nape, Dk. Bashiru waungana kukemea wanasiasa kushughulikiwa na Polisi

Spread the love

HATUA ya Dk. Bashiru Ally, Katibu Mkuu wa CCM  kukosoa vitendo vya baadhi ya Polisi kutumia nguvu katika kuwashughulikia wanasiasa, imemuibua Nape Nnauye, Mbunge wa Jimbo la Mtama. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Kupitia ukurasa wake wa Twitter leo tarehe 13 Julai 2019, Nape amenukuu taarifa ya Dk. Bashiru iliyochapishwa na gazeti la mtandao la Mwananchi na kueleza kwamba, huyo ndiye Dk. Bashiru anayemjua.

Nape ameandika ‘Huyu ndio Dr. Bashiru Ally ninayemjua.”

Jana tarehe 12 Julai 2019 akizungumza katika ziara yake kwenye mji wa Kibaya Wilaya ya Kiteto mkoani Manyara, Dk. Bashiru alisema Jeshi la Polisi likianza kutumia mabavu katika kutatua migogoro ya ndani, ni dalili ya kushindwa kuongoza nchi.

Dk. Bashiru amesema hakuna sababu ya  Jeshi la Polisi kutumia mabavu, wakati wananchi wanatii sheria bila shuruti.

Aidha, Dk. Bashiru amesema nguvu ya ziada ni vyema ikatumika pale ambapo wananchi hawatii sheria.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!