Tuesday , 5 December 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Nape, Dk. Bashiru waungana kukemea wanasiasa kushughulikiwa na Polisi
Habari za Siasa

Nape, Dk. Bashiru waungana kukemea wanasiasa kushughulikiwa na Polisi

Spread the love

HATUA ya Dk. Bashiru Ally, Katibu Mkuu wa CCM  kukosoa vitendo vya baadhi ya Polisi kutumia nguvu katika kuwashughulikia wanasiasa, imemuibua Nape Nnauye, Mbunge wa Jimbo la Mtama. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Kupitia ukurasa wake wa Twitter leo tarehe 13 Julai 2019, Nape amenukuu taarifa ya Dk. Bashiru iliyochapishwa na gazeti la mtandao la Mwananchi na kueleza kwamba, huyo ndiye Dk. Bashiru anayemjua.

Nape ameandika ‘Huyu ndio Dr. Bashiru Ally ninayemjua.”

Jana tarehe 12 Julai 2019 akizungumza katika ziara yake kwenye mji wa Kibaya Wilaya ya Kiteto mkoani Manyara, Dk. Bashiru alisema Jeshi la Polisi likianza kutumia mabavu katika kutatua migogoro ya ndani, ni dalili ya kushindwa kuongoza nchi.

Dk. Bashiru amesema hakuna sababu ya  Jeshi la Polisi kutumia mabavu, wakati wananchi wanatii sheria bila shuruti.

Aidha, Dk. Bashiru amesema nguvu ya ziada ni vyema ikatumika pale ambapo wananchi hawatii sheria.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Dk. Biteko: Viongozi tuache alama nzuri katika utendaji wetu

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za SiasaTangulizi

Chanzo maporomoko yaliyoua 65 Hanang, chatajwa

Spread the loveSERIKALI imesema kumeguka kwa sehemu ya Mlima Hanang ambao ilikuwa...

Habari za Siasa

Baba yake Ole Sabaya ashinda Uenyekiti CCM – Arusha

Spread the loveLoy Thomas Sabaya ambaye ni Baba wa aliyekuwa Mkuu wa...

Habari za Siasa

Serikali yaagiza uchunguzi chanzo maporomoko Hanang

Spread the loveSERIKALI imeagiza uchunguzi ufanyike ili kubaini chanzo cha maporomoko ya...

error: Content is protected !!