Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Mtandao wa Elimu waweka wazi malengo yake
Elimu

Mtandao wa Elimu waweka wazi malengo yake

Spread the love

CLEMENT Maganga, Mwakilishi wa Mratibu wa Mtandao wa Elimu Tanzania (Ten/Met), amesema kuwa mtandao wa elimu nchini imejiwekea malengo makuu matatu ya kuimarisha elimu. Anaripoti Danson Kaijage, Handeni … (endelea).

Kiongozi huyo akizungumza wananchi,wadau waelimu pamoja na wanafunzi wakati wa Uzinduzi wa maadhimisho wiki ya Elimu iliyofanyika kitaifa wilaya Handeni, Tanga, leo amesema kuwa malengo hayo matatu ni pamoja na kuongeza uelewa kwa umma juu ya haki elimu bora. 

Alitaja malengo mengine kuwa ni kuhamasisha serikali kuzingatia makundi yaliyokosa fursa kama wenye ulemavu, wito wa upatikanaji wa miundombinu na vifaa vya shule, mafunzo ya walimu ikiwa ni pamoja na walimu wenye ulemavu.

Maganga ameendelea kutaja malengo mengine ni kuhamasisha na kukumbusha jamii, Serikali na mashirika yasiyokuwa ya kiserikali kuhusu umuhimu wa uwajibikaji wa pamoja katika masuala ya elimu na utekelezaji wa malengo endelevu la nne na la tano.

“Mkoa wa Tanga hasa wilaya ya Handeni kumechaguliwa kuwa sehemu ya kufanyia maadhimisho kutokana na juhudi zanazofanywa na wilaya hasa katika upande wa Elimu jumuishi,” alieleza Maganga.

Kwa upande wa baadhi wanafunzi wa kike walisema kuwa wanakabiliana na changamoto mbalimbali ya kukatisha masomo ikiwa ni pamoja na miundombinu kutokuwa rafiki.

Wakizungumza na waandishi wa habari wanafunzi hao wa kike walisema umbali wa kati ya shule na nyumbani unachangia zaidi wanafunzi wa kike kurubuniwa na waendesha pikipiki maarufu mama bodaboda.

Hadija Omari ambaye ni mwanafunzi wa kike alisema changamoto nyingine ambayo wanafunzi wanatukana nayo ni pamoja na ukata unaotokana na familia zao kwa familia kushindwa kuwapatia mahitaji wanayoyataka.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Martin Shigella wakati akizindua maadhimisho ya wiki ya Elimu Kitaifa wilayani Handeni alisema kuwa serikali inatambua umuhimu wa asasi zisizokuwa za kiserikali zinavyokuza na kuhamasisha umuhimu wa elimu na ubora wa Elimu nchini.

Shigella alisema kuwa pamoja na mambo mengine mkoa umejiwekea malengo ya kuifanya elimu kuwa shirikishi kwa jamii ili kuhamikisha inapandisha kiwango cha ufaulu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari za Siasa

MbungeCCM ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the love  MBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze...

ElimuHabari za Siasa

Walimu 52,551 kupandishwa madaraja mwaka huu

Spread the loveNaibu Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala...

BiasharaElimu

NMB yatoa vifaa vya ujenzi kwa shule sita Nyasa  

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

error: Content is protected !!