Thursday , 9 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge wa Chadema awamwaga Polisi
Habari za Siasa

Mbunge wa Chadema awamwaga Polisi

Pascal Haonga, Mbunge wa Mbozi (mwenye kombati nyeusi) akiwa na wadau wengine wakishangilia
Spread the love

MBUNGE wa jimbo la Mbozi mkoani Songwe kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Pascal Haonga na wenzake wameshinda kesi iliyokuwa inawakabili katika Mahakama ya Wilaya ya Mbozi, baada ya upande wa mashtaka kushindwa kuthibitisha makosa dhidi ya watuhumiwa. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Haonga na wengine Katibu wake Wilfred Mwalusamba na Mashaka Mwampashi walikuwa wakikabiliwa na makosa ya kuvuruga mkutano wa uchaguzi wa baraza la mji mdogo wa Mlowo kosa la pili na la tatu kuwazuia askari kutekeleza majukumu yao makosa hayo wanadaiwa kuyatenda tarehe 28 Agosti, mwaka huu.

Akisoma hukumu hiyo, Hakimu Mfawidhi Nemes Chami alisema katika mashtaka yote matatu yalikuwa yanawakabili, hakuna hata sehemu moja upande wa mashtaka uliothibitisha.

“Hakuna mahali walipoonesha kwamba washtakiwa hawa waliwazuia askari kutekeleza majukumu yao na hakuna mahali walipo thibitisha kwamba washtakiwa walilazimisha kurudi ukumbini baada ya kutolewa nje” Alisema Chami.

Baada ya kusoma hukumu hiyo hakimu huyo alisema kuwa kama kuna upande ambao haujarizika na hukumu hiyo una haki ya kukata rufaa ndani ya muda.

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia: Matumizi ya nishati safi sio anasa, ladha ipo

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amesema matumizi ya nishati safi kwa...

Habari za SiasaTangulizi

Samia: Kuanzia Agosti marufuku kutumia mkaa, kuni

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amemuagiza Waziri wa Nchi, Ofisi ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mwendokasi Kigogo – Segerea kujengwa awamu ya 5

Spread the loveNaibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (TAMISEMI), Festo Dugange...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Rais Samia ni Mzanzibari: Shida Iko Wapi?

Spread the loveTAIFA linakabiliwa na upungufu wa fikra sahihi. Upungufu huu unaonekana...

error: Content is protected !!