Wednesday , 8 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa DPP awafutia mashtaka viongozi Bavicha waliosota rumande siku 170
Habari za Siasa

DPP awafutia mashtaka viongozi Bavicha waliosota rumande siku 170

Nusrat Hanje, Katibu wa BAVICHA
Spread the love

KATIBU Mkuu wa Baraza la Vijana la Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Bavicha), Nusrat Hanje, Mratibu wa Uhamasishaji wa baraza hilo, Twaha Mwaipaya na wenzao sita wameachiwa huru baada ya kufutiwa mashtaka yaliyokuwa yanawakabili katika Mahakama ya Mkoa wa Singida. Anaripoti Mwandishi Wetu, Singida … (endelea).

Hanje, Mwaipaya na Samwel Gishinde Malo, Katibu wa Chadema mkoani Singida na wengine watano walikamatwa na Jeshi la Polisi mkoani humo tarehe 6 Julai 2020 wakituhumiwa kufanya mikusanyiko isiyo halali.

Wanasiasa hao wameachiwa huru jana usiku Jumatatu tarehe 23 Novemba 2020, baada ya kusota rumande mkoani Singida kwa muda zaidi ya mitano sawa na siku 170.

Hanje, Mwaipaya na wenzao walifunguliwa Kesi ya Jinai Namba 115/2020, katika Mahakama ya Mkoa wa Singida wakikabiliwa na mashtaka manne ikiwemo mkusanyiko usio halali, kudharau wimbo na bendera ya taifa.

Biswalo Mganga, Mkurugenzi wa Mashtaka Tanzania (DPP)

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Chadema katika ukurasa wake wa Twitter, viongozi hao wa Bavicha wameachiwa usiku wa jana tarehe 23 Novemba 2020 baada ya Mkurgenzi wa Mashtaka (DPP) kuwafutia mashtaka.

“Katibu Mkuu wa Bavicha Nusrat Hanje na Mratibu wa uhamasishaji Bavicha Taifa Twaha Mwaipaya na wenzao sita wameachiwa huru usiku huu. Upande wa Jamhuri hawapo tayari kuendelea na kesi, hivyo wamefutiwa mashtaka yao,” inaeleza taarifa hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia: Matumizi ya nishati safi sio anasa, ladha ipo

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amesema matumizi ya nishati safi kwa...

Habari za SiasaTangulizi

Samia: Kuanzia Agosti marufuku kutumia mkaa, kuni

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amemuagiza Waziri wa Nchi, Ofisi ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mwendokasi Kigogo – Segerea kujengwa awamu ya 5

Spread the loveNaibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (TAMISEMI), Festo Dugange...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Rais Samia ni Mzanzibari: Shida Iko Wapi?

Spread the loveTAIFA linakabiliwa na upungufu wa fikra sahihi. Upungufu huu unaonekana...

error: Content is protected !!