Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa DPP awafutia mashtaka viongozi Bavicha waliosota rumande siku 170
Habari za Siasa

DPP awafutia mashtaka viongozi Bavicha waliosota rumande siku 170

Nusrat Hanje, Katibu wa BAVICHA
Spread the love

KATIBU Mkuu wa Baraza la Vijana la Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Bavicha), Nusrat Hanje, Mratibu wa Uhamasishaji wa baraza hilo, Twaha Mwaipaya na wenzao sita wameachiwa huru baada ya kufutiwa mashtaka yaliyokuwa yanawakabili katika Mahakama ya Mkoa wa Singida. Anaripoti Mwandishi Wetu, Singida … (endelea).

Hanje, Mwaipaya na Samwel Gishinde Malo, Katibu wa Chadema mkoani Singida na wengine watano walikamatwa na Jeshi la Polisi mkoani humo tarehe 6 Julai 2020 wakituhumiwa kufanya mikusanyiko isiyo halali.

Wanasiasa hao wameachiwa huru jana usiku Jumatatu tarehe 23 Novemba 2020, baada ya kusota rumande mkoani Singida kwa muda zaidi ya mitano sawa na siku 170.

Hanje, Mwaipaya na wenzao walifunguliwa Kesi ya Jinai Namba 115/2020, katika Mahakama ya Mkoa wa Singida wakikabiliwa na mashtaka manne ikiwemo mkusanyiko usio halali, kudharau wimbo na bendera ya taifa.

Biswalo Mganga, Mkurugenzi wa Mashtaka Tanzania (DPP)

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Chadema katika ukurasa wake wa Twitter, viongozi hao wa Bavicha wameachiwa usiku wa jana tarehe 23 Novemba 2020 baada ya Mkurgenzi wa Mashtaka (DPP) kuwafutia mashtaka.

“Katibu Mkuu wa Bavicha Nusrat Hanje na Mratibu wa uhamasishaji Bavicha Taifa Twaha Mwaipaya na wenzao sita wameachiwa huru usiku huu. Upande wa Jamhuri hawapo tayari kuendelea na kesi, hivyo wamefutiwa mashtaka yao,” inaeleza taarifa hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!