Wednesday , 8 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Anna Mgwira kumrithi Meck Sadick
Habari za Siasa

Anna Mgwira kumrithi Meck Sadick

Anna Mgwira, Mwenyekiti wa ACT-Wazalendo
Spread the love

JOHN Magufuli, Rais wa Tanzania amemteua Anna Mgwira, Mwenyekiti wa Chama cha ACT-Wazalendo kuwa Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro, anaandika Hamisi Mguta.

Mgwira ambaye alikuwa mmoja wa wapinzani wa Rais Magufuli katika uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 anachukua nafasi hiyo iliyoachwa na Said Meck Sadick aliyekuwa mkuu wa mkoa huo ambaye alijiuzulu nafasi hiyo.

Wakati huo huo, Rais amemteua Meja Jenerali Issah Suleiman Nassor aliyekuwa Mkuu wa Oparesheni ya Mafunzo wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) kuwa balozi.

Pia amemteua DIGP Abdulrahman Kaniki aliyekuwa Naibu Mkuu wa Jeshi la Polisi kuwa balozi. Hata hivyo tarehe ya kuapishwa kwao bado haijatangazwa rasmi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia: Matumizi ya nishati safi sio anasa, ladha ipo

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amesema matumizi ya nishati safi kwa...

Habari za SiasaTangulizi

Samia: Kuanzia Agosti marufuku kutumia mkaa, kuni

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amemuagiza Waziri wa Nchi, Ofisi ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mwendokasi Kigogo – Segerea kujengwa awamu ya 5

Spread the loveNaibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (TAMISEMI), Festo Dugange...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Rais Samia ni Mzanzibari: Shida Iko Wapi?

Spread the loveTAIFA linakabiliwa na upungufu wa fikra sahihi. Upungufu huu unaonekana...

error: Content is protected !!