Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Bavicha wamlaani Ndugai
Habari za SiasaTangulizi

Bavicha wamlaani Ndugai

Job Ndugai,. Spika wa Bunge la Tanzania
Spread the love

SIKU moja baada ya Spika wa Bunge la Tanzania Job Ndugai, kumtoa kwa nguvu Waziri Kivuli wa Wizara ya Nishati na Madini, John Mnyika, Baraza la Vijana Chadema (Bavicha), limeaalani  kitendo hicho cha udhalilishaji kilichofanywa na  Spika, anaandika Hamisi Mguta.

Mnyika ambaye pia ni Mbunge wa Kibamba aliamuliwa jana kutoka nje ya Bunge na kutohudhuria vikao saba vya bunge vinavyoendelea kutokana na kilichoitwa na spika kuwa ni utovu wa nidhamu uliofanywa na Mnyika kwa kubishana na kiti baada ya kutokea malumbano kati yake na spika.

Patrobas Katabi, Mwenyekiti wa Bavicha, akizungumza na wanahabari leo katika makao makuu ya chama hicho Kinondoni ameeleza kuwa Ndugai hakutumia busara kumtoa Mnyika bali alikuwa na jazba katika kutoa uamuzi huo.

“Tunasikitika na kitendo kilichofanywa na Ndugai, nadhani busara alizisahau nyumbani basi angejaribu hata kuzikumbuka kuliko kutoa uamuzi kama ule.

“Adhabu ya Mnyika kutoka nje ya Bunge ilitosha kabisa. Lakini si kumwambia asihudhurie vikao kwa siku kadhaa, ni wakati muafaka wa Ndugai kufanya upya marejeo ya uamuzi aliyoutoa ambao anadai ulikuwa wa jazba kuliko busara,” amesema Katambi.

Katambi amesema vita ya madini haiwezi kufanikiwa kwa kuwatoa  wapinzani nje ya Bunge ambao wana mawazo mbadala ambayo yanaweza kuwasaidia kwa namna moja au nyingine.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!