Monday , 5 June 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Anna Mgwira kumrithi Meck Sadick
Habari za Siasa

Anna Mgwira kumrithi Meck Sadick

Anna Mgwira, Mwenyekiti wa ACT-Wazalendo
Spread the love

JOHN Magufuli, Rais wa Tanzania amemteua Anna Mgwira, Mwenyekiti wa Chama cha ACT-Wazalendo kuwa Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro, anaandika Hamisi Mguta.

Mgwira ambaye alikuwa mmoja wa wapinzani wa Rais Magufuli katika uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 anachukua nafasi hiyo iliyoachwa na Said Meck Sadick aliyekuwa mkuu wa mkoa huo ambaye alijiuzulu nafasi hiyo.

Wakati huo huo, Rais amemteua Meja Jenerali Issah Suleiman Nassor aliyekuwa Mkuu wa Oparesheni ya Mafunzo wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) kuwa balozi.

Pia amemteua DIGP Abdulrahman Kaniki aliyekuwa Naibu Mkuu wa Jeshi la Polisi kuwa balozi. Hata hivyo tarehe ya kuapishwa kwao bado haijatangazwa rasmi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Lusinde: CCM hatuliachii ng’o jimbo la Moshi Mjini

Spread the loveMJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC), Livingston...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar: Bakharesa hajavamia shamba letu

Spread the love  IKULU Visiwani Zanzibar, imeeleza kuwa eneo la kiwanda cha...

Habari za SiasaTangulizi

Zanzibar watangaza rasmi kuwa shamba la Razaba ni mali yao

Spread the love  SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), imetangaza rasmi kwamba shamba...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Mwinyi azindua Kamati ya Maridhiano Visiwani

Spread the love  RAIS wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Dk. Hussein...

error: Content is protected !!