ZITTO Kabwe, Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, ameeleza sababu 10 za kuking’oa Chama cha Mapinduzi (CCM), katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).
Zitto ametaja sababu hizo wakati akifungua mkutano mkuu wa chama hicho, leo tarehe 14 Machi 2020, jijini Dar es Salaam, Zitto
Miongoni mwa sababu alizotaja Zitto ni, CCM kupasuka kutokana na kundi kubwa la chama hicho, kuchoshwa na vitendo vya ubabe, huku nyingine ikiwa ni mdororo wa uchumi wa taifa na wa wananchi.
“CCM imo vipande vipande, kundi kubwa limechoshwa na ubabe. Katika kipindi cha udikteta, CCM imeshaharibu uchumi wa nchi, imefukarisha wananchi. CCM haipaswi kukaa madarakani hata kwa mwezi mmoja,” amedai Zitto.
Sababu nyingine alizotaja Zitto ni, CCM kushindwa kutekeleza ahadi zake kwa wananchi, pamoja na kukosa mbinu za kuwakwamua wananchi katika ufukara.
“CCM chama laghai, hakitimizi ahadi zake, Watanzania hawawezi kukubali kufanywa watoto wadogo. Pia, imeshiwa mbinu na maarifa katika kukwamua Watanzania kwenye umasikini,” amesema Zitto.
Pia, Zitto amesema kudorola kwa sekta ya elimu kutokana na utekelezaji wa sera mbovu, kutasaidia ACT-Wazalendo kuiangusha CCM katika uchaguzi ujao.
“Utekelezaji sera elimu bure umeanza kubainika umetoa elimu bure. Elimu inazidi kuporomoka, wanafunzi walioahidiwa mikopo wanafukuzwa kwa kudai mikopo,” amesema Zitto.
Sababu nyingine alizotaja Zitto ni “CCM haina mkakati wa kutatua changamoto ya ajira, kupitia sera mbovu za CCM maisha ya Watanzania yamekuwa magumu, hifadhi ya chakula inatosha kwa siku mbili.”
Leave a comment