Monday , 6 May 2024
Home Habari Mchanganyiko ZIC yawahakikishia usalama wawekezaji Dubai
Habari Mchanganyiko

ZIC yawahakikishia usalama wawekezaji Dubai

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la (ZIC), Arafat Haji
Spread the love

SHIRIKA la Bima Zanzibar (ZIC) limewakaribisha wawekezaji Visiwani Zanzibar kuwekeza kwa kuwahakikishia usalama wa uwekezaji na mali zao wakati wote wakiwepo Visiwani humo. Anaripoti Matilda Buguye, Zanzibar … (endelea). 

Hayo yameelezwa jana tarehe 25 Februari, 2022 na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la (ZIC), Arafat Haji katika maonesho ya Biashara Kimataifa yanayoendelea katika Falme za Kiarabu-Dubai.

Haji amewakaribisha wadau kuwekeza Visiwani Zanzibar na kupitia Shirika hilo kwani wana uzoefu na masuala ya bima za aina mbalimbali.

“Wawekezaji tunawapa elimu ya namna gani wataweza kuwa na uwekezaji wenye usalama na kuhakikisha kunakua na ajira ya muda mrefu ili kuleta tija na kukuza uchumi na maslahi ya Taifa,” amesema.

Aidha, Haji ameeleza kuwa wawekezaji wanapoamua kushirikisha ZIC wanafanya maamuzi sahihi kwani wapo tayari kuwapa miongozo ya kusimamia uwekezaji huo na kuhakikisha mitaji yao inaleta manufaa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Serikali kuwakopesha wajasiriamali 18.5bn/- kupitia NMB

Spread the loveSerikali imetenga kiasi cha Sh 18.5 bilioni kwa ajili ya...

AfyaHabari Mchanganyiko

Huduma za kibingwa zazinduliwa katika hospitali za halmashauri 184

Spread the loveSERIKALI imezindua huduma za matibabu za kibingwa katika hospitali 184...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

Habari Mchanganyiko

Prof. Mbarawa aanika mafanikio ya TMA

Spread the loveSHUGHULI za Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), zimeimarika...

error: Content is protected !!