Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Wajasiriamali washauriwa kuwa na Bima ya biashara
Habari Mchanganyiko

Wajasiriamali washauriwa kuwa na Bima ya biashara

Spread the love

WAJASIRIAMALI nchini wanatakiwa kuwa na bima za biashara ili wanapopatwa na majanga mbalimbali yakiwemo moto,ugonjwa waweze kufidiwa. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Hayo yalielezwa Jana na Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Bima ya Fortis, Maryam Shamo alipokua akizungumza na waandishi wa habar wakati wa uzinduzi wa Malkia Bima uliofanyika jijini Dar es Salaam.

Fortis kwa kushirikiana na Assemblies Bima Jana walizindua huduma ya Malkia akaunti kwa lengo la kujinufaisha mjasiriamali mwanamke kufikia malengo yake akiwa na ulinzi wa Bima hiyo.

Maryam alisema kuwa Fortis kwa kushirikiana Assemble imeamua kufanya hivi kwa lengo la kuwanufaisha wanawake mmoja mmoja au kwenye vikundi.

“Wanawake kwenye vikundi kwa kama vile vikoba,saccos ,vikundi vya akina mama na wafanyabiashara wanapopata maafa yanayosababishwa na moto na viashiria vya hatari zake,kukatizwa kwa biashara kunakotokana na moto au kuvamiwa na majambazi,” alisema Maryam.

Alisema Malkia Bima inafaida kubwa ikiwa ni pamoja na ushauri wa afya baada ya maafa ya moto,gari wagonjwa pindi ajali ya moto inapotokea ,ajali binafsi,kulipiwa fedha hospital pindi mtu anapopatwa na maradhi na huduma nyinginezo.

Ameeleza kuwa Malkia.linda akaunti ni rahisi kufungua na inagharimu kiasi cha shilingi 8000 tu.

Naye Tabia Massudi Mkurugenzi wa Bima ya Inssuarance alisema wameamua kuungana pamoja ili kuunga mkono jitihada za serikali kwamba kila mtanzania awe na Bma.

Hata hivyo alisema licha ya kwamba boma anajulikana kama Malkia lakini kila mjasiriamali anufaike nayo mwanamke na mwanaume

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!