Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Tangulizi Wema Sepetu afungiwa muda usiojulikana
Tangulizi

Wema Sepetu afungiwa muda usiojulikana

Wema Sepetu
Spread the love

ALIYEKUWA Miss Tanzania mwaka 2006, Wema Sepetu amefungiwa kwa muda usiojulikana kujishughulisha na filamu na uigizaji, na Bodi ya Filamu Tanzania. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea)

Bodi ya Filamu imemtia kifungoni Wema kufuatia picha zake chafu zilizosambaa hivi karibuni kwenye mitandao ya kijamii, akiwa faragha na mwanamme anayedaiwa kuwa mume wake mtarajiwa.

Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu, Joyce Fisoo akizungumza na wanahabari baada ya kumhoji Wema leo tarehe 26 Oktoba 2018, amesema bodi hiyo imejiridhisha pasipo shaka kwamba Wema amelidhalilisha taifa, na kwamba kufuatia ukiukwaji huo imechukua hatua ya kumfungia.

Fisoo amesema licha ya adhabu hiyo, Bodi ya Filamu itafuatilia kwa karibu mwenendo wa Wema Sepetu na kwamba itamuondoa kifungoni itakapojiridhisha kuwa amejirekebisha.

“Wema amelidhalilisha taifa, kuwafanya watazamaji kuiga tabia, mwenendo, desturi na maadili yasiyo faa na wakiuke maadili yasiyokuwa ya kitanzania. Na kudhalilisha Tanzania kwa ujumla.

Kufuatia ukiukwaji huo imejiridhisha pasipo shaka na kuchukua hatua ya kumfungia Wema Sepetu kutojihusisha na masuala ya filamu na uigizaji hadi pale bodi itakapojiridhisha kwamba amejirekebisha, na itafuatilia kwa karibu mwenendo wake,” amesema na kuongeza Fisoo.

“Kufuatia kukiri makosa yake na kuomba radhi kwa maandishi kwa bodi ya filamu na watanzania kwa ujumla na kuonyesha kwamba anajutia kosa lake ni imani kwamba hatorudia.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za SiasaTangulizi

Shibuda amlima waraka mzito Bulembo

Spread the loveMKONGWE wa siasa nchini, John Shibuda amemshukia kada maarufu wa...

error: Content is protected !!