Tuesday , 21 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Mwanafunzi aliyetumbukia chooni aokolewa, Polisi kuchunguza
Habari MchanganyikoTangulizi

Mwanafunzi aliyetumbukia chooni aokolewa, Polisi kuchunguza

Spread the love

MWANAFUNZI wa darasa la kwanza katika Shule ya Msingi Seliani iliyoko wilayani Arusha, Emanuel Zacharia amenusurika kifo baada ya kutumbukia katika shimo la choo cha shule hiyo. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, SACP Ramadhan Ng’azi amethibitisha tukio hilo akisema kuwa, lilitokea asubuhi ya leo tarehe 26 Oktoba 2018, majira ya saa tatu na nusu asubuhi.

Akizungumza na mtandao huu, Kamanda Ng’azi ameeleza kuwa, Zacharia alipatwa na mkasa huo alipokwenda chooni kujisaidia, ambapo isivyo bahati shimo la choo lilitumbukia.

Ameeleza kuwa, baada ya tukio hilo kutokea, wananchi, waalimu na polisi walifanya jitihada za kumuokoa mwanafunzi huyo ambaye kwa sasa yuko katika Hospitali ya Seliani akipatiwa matibabu.

Kamanda Ng’azi amesema Jeshi la Polisi linachunguza chanzo cha tukio hilo, na kutoa saa tatu kwa uongozi wa shule hiyo kufanya marekebisho ya choo hicho.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Tanzania yakabidhi rasmi msaada nchini Malawi

Spread the loveWAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,...

Habari Mchanganyiko

Bashe: Tumeshagawa pikipiki 5,500 kati ya 7,000 kwa maafisa ugani

Spread the love  WAZIRI wa Kilimo, Hussen Bashe, amesema wizara hiyo tayari...

Habari Mchanganyiko

Spika Tulia awapa neno mawaziri utekelezaji mashamba ya pamoja

Spread the love  SPIKA wa Bunge, Dk. Tulia Ackson, amewataka mawaziri kushirikiana...

Habari Mchanganyiko

Ukosefu wa maadili kwa wakunga, wauguzi bado changamoto

Spread the loveIMEELEZWA kuwa vitendo vya uvunjifu wa maadili kwa  wauguzi na...

error: Content is protected !!