Tuesday , 3 October 2023
Home Habari Mchanganyiko Waziri Ndugulile atoa maagizo TCRA
Habari MchanganyikoTangulizi

Waziri Ndugulile atoa maagizo TCRA

Spread the love

WAZIRI wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari (Tehama), Dk. Faustine Ndugulile ameitaka, Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), kuboresha mifumo mbalimbali ya usimamizi wa huduma za mawasiliano ili kuhakikisha usalama na ubora wa huduma nchini, unakuwepo. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Dk. Ndugulile, alitoa maagizo hayo mwishoni mwa wiki, mara baada ya kutembelea mifumo hiyo makao makuu ya TCRA mkoani Dar es Salaam na kupokewa na viongozi mbalimbali wa mamlaka hiyo akiwemo Mkurugenzi wake Mkuu, Dk. Jabiri Bakari.

Alisema wananchi wanatarajia kupata huduma bora zenye usalama.

“Upatikanaji wa huduma bora, za uhakika na salama ni jambo la msingi sana kwa ajili ya maendeleo ya wananchi na Taifa” alisema Dk. Ndugulile.

 

Waziri huyo, aliipongeza TCRA kwa ubunifu wa kujenga mifumo wezeshi kwa huduma mbalimbali za mawasiliano nchini, ambapo uboreshaji wake ni muhimu.

Baadhi ya mifumo aliyotembelea ni Mfumo wa Usimalizi na Udhibiti wa Masafa ya Redio na Televisheni na Kituo cha Kuratibu Majanga ya Kimtandao (TZ-CERT).

TZ-CERT pia itatoa ushuri wa kitaalam namna bora wa kudhibiti na kupambana ya majanga mbalimbali ya kimtandao kwa taasisi na makampuni mbalimbali nchini Tanzania.

Waziri pia alitembelea kituo cha huduma kwa wateja ambapo alihimiza TCRA kuendeza kushirikiana na taasisi zingine zikiwemo za kiudhibiti kama Banki Kuu ya Tanzania (BoT).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wawili wanaswa wakitengeneza noti bandia

Spread the loveJESHI la Polisi mkoani Songwe limewakamata watu wawili kwa tuhuza...

AfyaHabari Mchanganyiko

Chanjo mpya ya malaria Sh 5,000-10,000

Spread the loveShirika la afya la Duniani (WHO) limeridhia chanjo ya pili...

AfyaHabari Mchanganyiko

Wagonjwa kiharusi waongezeka, Hospitali Mkapa yaja matibabu mapya

Spread the loveHOSPITALI ya Benjamini Mkapa kwa kushirikiana na madaktari Bingwa kutoka...

Habari Mchanganyiko

Wananchi waamua kujenga zahanati kukwepa adha kufuata huduma mbali

Spread the loveWANANCHI wa Kijiji cha Kwikerege, kilichopo katika Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!