Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Wawili wafa mgodini wakichimba dhahabu
Habari Mchanganyiko

Wawili wafa mgodini wakichimba dhahabu

Spread the love

 

WATU wawili wamefariki duniani na wengine sita kuokolewa wakiwa hai baada ya duara walilokuwa wakichimba madini ya dhahabu kutitia katika Mgodi wa Wachapakazi uliopo Kijiji cha Nyandolwa wilaya ya Shinyanga mkoani Shinyanga. Anaripoti Paul Kayanda – Shinyanga. (endelea…)

Miili ya watu hao iliokolewa kwa nyakati tofauti katika zoezi la uokoaji lililodumu kwa muda wa siku 14 kuanzia tarehe 15 Septemba hadi 1 Oktoba mwaka huu ambapo mwili wa pili ulipatikana.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo, Mmoja kati ya wakurugenzi wa mgodi huo, Joseph Makoba amesema  baada ya ajali hiyo kutokea na kufanya uokoaji, walibaini watu wawili wamesalia.

“Huwa tuna takwimu za watu wanainga shimoni kufanya kazi. Takwimu zilionesha wamebaki wawili hivyo tulianza kuwatafuta kama binadamu wenzetu na nguvu kazi.

“Baada ya siku nne kupitas tulifanikiwa kupata mwili wa kijan a mmoja ambaye ni mkazi wa Nyang’wale kisha siku iliyofuata tukampata wa mwisho ambaye alikuwa mkazi wa Segese. Wote tayari tumewasitiri kwenye nyumba zao za milele.

“Suala la msingi kwetu ni usalama kwanza lakini hizi ni ajali  kama ajali nyingine hivyo tunaendelea kuzidisha juhudi kuhakikisha usalama unazidi kuimarishwa ndani ya mgodi,” amesema.

Aidha, mmoja wa  mashuhuda wa tukio hilo Jastine Siyaraha ameuomba uongozi wa mgodi huo kuimarisha suala la usalama mgodini ili yasitokee matukio ya aina hiyo mara kwa mara.

“Mimi ni mfanyakazi wa mgodi huu, tangu ajali itokee mgodi umefungwa, hivyo tumeathirika sana kiuchumi hasa ikizingatiwa tunategemea shughuli za uchimbaji wa madini kuendesha maisha yetu,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!