Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Wanafunzi waliofanya mtihani wakiwa na watoto wachanga wamkuna Jokate
ElimuHabari za Siasa

Wanafunzi waliofanya mtihani wakiwa na watoto wachanga wamkuna Jokate

Spread the love

KATIBU Mkuu wa Jumuiya ya Wanawake Tanzani (UWT), Jokate Mwegelo amesema hatua ya wanafunzi walioruhusiwa kufanya mitihani ya kidato cha nne mwaka 2023 huku wakiwa na watoto wachanga, ni uamuzi wa kipekee ambao umefufua ndoto za mabinti hao. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Amesema uamuzi huo ambao uliasisiwa na Rais Samia Suluhu Hassan, umelenga katika kuhakikisha kila mwanafunzi anatimiza ndoto yake kupitia elimu.

Joketi ametoa kauli hiyo leo Jumamosi alipotembelea eneo la Chamazi Magengeni Jijini Dar es salaam na kukutana na binti aliyefanya mitihani ya kidato cha nne mwaka 2023 huku akiwa ananyonyesha.

Mbali na binti huyo, pia Jokate amekutana na binti mwingine anayeishi maeneo ya Mbande Jijini Dar es salaam ambaye na yeye amefanya mitihani huku akiwa ananyonyesha mtoto mwenye siku nane.

Aidha, mbali na kuwapongeza kwa jitihada za kufanya mtihani huo, Joketi pia ametoa wito kwa wazazi kuzingatia malezi bora ya watoto ili kuwaepusha na mimba za utotoni.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!