KATIBU Mkuu wa Jumuiya ya Wanawake Tanzani (UWT), Jokate Mwegelo amesema hatua ya wanafunzi walioruhusiwa kufanya mitihani ya kidato cha nne mwaka 2023 huku wakiwa na watoto wachanga, ni uamuzi wa kipekee ambao umefufua ndoto za mabinti hao. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).
Amesema uamuzi huo ambao uliasisiwa na Rais Samia Suluhu Hassan, umelenga katika kuhakikisha kila mwanafunzi anatimiza ndoto yake kupitia elimu.
Joketi ametoa kauli hiyo leo Jumamosi alipotembelea eneo la Chamazi Magengeni Jijini Dar es salaam na kukutana na binti aliyefanya mitihani ya kidato cha nne mwaka 2023 huku akiwa ananyonyesha.
Mbali na binti huyo, pia Jokate amekutana na binti mwingine anayeishi maeneo ya Mbande Jijini Dar es salaam ambaye na yeye amefanya mitihani huku akiwa ananyonyesha mtoto mwenye siku nane.
Aidha, mbali na kuwapongeza kwa jitihada za kufanya mtihani huo, Joketi pia ametoa wito kwa wazazi kuzingatia malezi bora ya watoto ili kuwaepusha na mimba za utotoni.
Leave a comment