Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Biashara Wamachinga Kivule walianzisha
Biashara

Wamachinga Kivule walianzisha

Spread the love

SAKATA la wafanyabiashara ndogondogo (wamachinga) eneo la Kivule kuvunjiwa na vibanda vyao Kisha mali kuchukuliwa na mgambo limechukua sura mpya baada ya kuzifuatilia na kuzikuta Ofisi za Jiji la Ilala zikiwa pungufu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Jana Jumapili, wakizungumza na waandishi wa habari, wamachinga hao wamemtaka Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Edward Mpogolo, ahakikishe mali zao wanazipata la sivyo watalifikisha sakata hilo kwa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan.

Baadhi ya wafanyabiashara wamedai kuwa, katika nyakati tofauti walifika ofisini hapo wakiwa na matumaini ya kupata mali zao zote, lakini jambo la kushangaza wamekuta baadhi ya mali hazipo.

Bihimba Mpaya, alidai “tunaishukuru Serikali kwa kuanza kushughulikia suala hilo, lakini tunashangaa kuona kwamba wafanyabiashara wanapata mali pungufu. Tunamtaka Mkuu wa Wilaya atuambie mali ziko wapi, lakini hao waliozichukua wanawajibishwaje.”

Kaimu Mwenyekiti wa wafanyabiashara hao, aliyejitambulishwa kwa jina la Swaleh, alimuomba Rais Samia aingilie Kati ili mali zao zipatikane.

Wafanyabiashara hao wamechukua hatua hiyo baada ya ziara ya Mpogolo, alyefika eneo hilo wiki iliyopita kushuhudia uharibifu huo na kuagiza hatua zaidi kuchukuliwa kwa wahusika, huku akikana kwamba sio maagizo ya Serikali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Biashara

Cheza sloti ya Zombie Apocalypse na ushinde kirahisi

Spread the love Wengi wetu hupenda filamu za Mazombie huwa zinatishakidogo lakini...

Biashara

Ushirikishwaji wa wafanyakazi ni muhimu katika utekelezaji wa sera za afya na usalama kazini

Spread the love  KILA ifikapo Aprili 28 ya kila mwaka, dunia huadhimisha...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Biashara

Wazir Jr kinara wa ufungaji KMC FC ajiunga Meridianbet

Spread the love    MUITE Wazir Jr ‘The King of CCM Kirumba’,...

error: Content is protected !!