UMOJA wa Wafanyabiashara wa Gesi (LPG) za Mitungi ya Majumbani nchini (TZLPGA) wamekutana na waandishi wa habari kujadili njia endelevu za kukuza sektahio kupitia uwezeshaji wa taarifa. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Umoja huo ulioanzishwa mwaka 2023 unaundwa na kampuni sita zinazofanya biashara ya gesi za mitungi kwa matumizi yamajumbani ambazo ni CAMGAS, O-GAS, LAKE GAS, TAIFA GAS, ORYX GAS, MANJI GAS na PUMA ENERGY.
Akizungumza na waandishi wa habari waliohudhuria mjadalahuo, Mkurugenzi Mkuu wa umoja huo, Amos Jackson alinukuliwa, ‘tunaamini kuwa ukusanyaji na usambazaji wataarifa sahihi kwenye sekta hii utasaidi kuleta mageuzimakubwa kwenye kufanikisha azma ya nchi yetu kupiga hatuakwenye matumizi ya gesi za mitungi majumbani.
Kwa hiyo uwepo wenu hapa utasaidia sana kupanua ufahamu wetukupitia maoni yenu kama wadau muhimu wa sekta hii’.
Amos alisema kuhusu mikakati iliyowekwa na umoja huo, alisema, ‘tumedhamiria kupanua matumizi ya teknolojiahii ya gesi za majumbani katika katika kupunguza uzalishajiwa kaboni, kuboresha ufanisi wa nishati, na kurahisishamatumizi mbadala za nishati safi’.
Aidha, Mwenyekiti wa TZLPGA, Benoit Araman alisisita umuhimu wa kudumisha ushirikiano baina ya wadauwa sekta hio na serikali.
Alisema, ‘ni wajibu wetu kuiungamkono serikali kuhakikisha tunaleta mapinduzi kwenye sektahii ya gesi majumbani ili kutokomeza uharibifu wa mazingiraunatokokana na matumizi ya mkaa’.
Aliendelea, ‘mkaa nitishio kwa maana huchangia kutengeneza hewa ya kaboniambayo inachafua mazingira na kuleta mabadiliko hasi yatabia ya nchi’.
Mdhahalo huo uliohudhuriwa na mgeni rasmi, Mkurugenzi Mkuu wa EWURA, Dk. James Andilile ambae ameungamkono uzinduzi wa kampeni wa kusambaza taarifa sahihi juuya matumizi salama ya gesi (LPG) kwa manufaa ya taifa kwaujumla.
TZLPGA imeahidi kushirikiana na wadau wa sekta hio kutoamsukumo wa wawekezaji kutoa pesa kwa ajili ya kukuzamatumizi ya nishati safi na athari zingine chanyazitakazosaidia kuwa tija kwa sekta ya nishati kwa ajili yamaendeleo ya Taifa zima.
Leave a comment