Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbowe: Nimempoteza rafiki hodari wa mabadiliko
Habari za SiasaTangulizi

Mbowe: Nimempoteza rafiki hodari wa mabadiliko

Spread the love

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadem), Freeman Mbowe ameeleza kupokea kwa mshtuko na majonzi makubwa taarifa za kifo cha Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowassa. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Amesema amepoteza rafiki, ndugu na mshauri mzuri lakini pia Tanzania na dunia imepoteza kiongozi shujaa, mwenye mchango mkubwa katika kujenga amani, ushirikiano na ustawi wa jamii.


Katika taarifa aliyoitoa kwa umma leo Jumapili, Mbowe amesema Lowassa alikuwa kiongozi shupavu, mwanasiasa mahiri, mwanaharakati hodari na alikuwa mstari wa mbele katika kupigania mabadiliko ya kisiasa na kiuchumi nchini mwetu.

“Alikuwa rafiki yangu na mshirika katika safari ya kuleta demokrasia ya kweli Tanzania. Alikuwa mtu mwenye hekima, busara, ujasiri, uzalendo, mtu mwenye huruma, upendo na msamaha kwa wote. Alikuwa mtu mwenye maono, mipango na mtekelezaji mzuri wa miradi mbalimbali ya maendeleo kwa manufaa ya wananchi.

Kwa niaba ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na Watanzania wenzangu, napenda kutoa salamu zangu za dhati, za Pole kwa familia, ndugu, jamaa, marafiki na wapenda demokrasia wote kwa kifo chake.

“Namuomba Mwenyezi Mungu aiweke roho yake mahali pema peponi, amsamehe makosa yake na amjaalie rehema zake. Mungu aipe faraja, nguvu na subira familia yake, chama chake, wafuasi wake na wote walioguswa na msiba huu,” amesema.

Amesema wataendelea kuenzi kazi, mawazo na hekima alizotuachia Mheshimiwa Lowassa. Pia wataendelea kumuombea na kumkumbuka kwa mema aliyotutendea.

“Mungu ailaze roho ya Mheshimiwa Edward Ngoyai Lowassa mahali pema peponi. Amina,” amesema Mbowe.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jacob, Malisa waachiwa kwa masharti

Spread the love  JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

error: Content is protected !!