Monday , 6 May 2024
Home Kitengo Maisha Afya Ummy Mwalimu aunda kamati kuchunguza malalamiko ya madaktari waliofelishwa
Afya

Ummy Mwalimu aunda kamati kuchunguza malalamiko ya madaktari waliofelishwa

Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu
Spread the love

Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu leo Jumatatu ametangaza ameunda Kamati huru yenye wajumbe 13 ili kuchunguza malalamiko ya madaktari watarajali (Intern Doctors) kuhusu kufeli mitihani ya kabla na baada ya mafunzo ya Internship ili waweze kupata usajili wa kudumu wa Baraza la Madaktari Tanganyika-MCT.

Kamati hiyo itafanya kazi kwa kipindi cha mwezi mmoja na kufuata hadidu za rejea zilizoainishwa na Wizara ili kuchunguza msingi wa malalamiko yaliyotolewa na Madaktari tarajali katika barua yao waliyoielekeza kwa Rais Samia Suluhu Hassan. Anaripoti Maryam Mudhihir …(endelea).

Kwa mujibu wa taarifa yake Waziri wa Afya,  iliyotumwa kwenye vyombo vya habari leo tarehe 14 Agosti 2023 amesema kuwa kamati hiyo huru itaongozwa na Mganga Mkuu wa Serikali Mstaafu, Profesa Mohamed Bakari.

“Kamati hiyo itafanya kazi kwa kipindi cha mwezi mmoja na kufuata hadidu za rejea zilizoainishwa na Wizara ili kuchunguza msingi wa malalamiko yaliyotolewa na Madaktari tarajali katika barua yao waliyoielekeza kwa Rais Samia Suluhu” imeeleza taarifa hiyo.

MCT inatekeleza wajibu wa  sheria ya madaktari,madaktari wa meno na wataalamu wa Afya shirikishi ,sura 152 ya mwaka 217, pamoja na kanuni zake za mitihani na usajili za mwaka 2018.

Sheria mpya inahitaji mtihani wa usajili wa muda ili kuhakikisha kuwa madaktari wanaopata umahiri husika kutoka Desemba 2020 hadi Desemba 2022 ambapo asilimia 68 hadi 99 ya madaktari wanaofanya mitihani hiyo wamefaulu.

Hata hivyo, katika mtihani wa Machi 2023, ni asilimia 42 tu ya watahiniwa 640 waliofaulu.

Taarifa hiyo inaeleza kuwa “Kamati itafanya kazi kwa muda wa mwezi mmoja na kutoa mapendekezo ya kutatua changamoto zilizobainika.

Wajumbe wa kamati ni wanataaluma wenye uzoefu katika sekta ya afya kutoka vyuo vikuu na hospitali”

Waziri Ummy amesema kuwa wakati kamati inatekeleza majukumu yake, mafunzo ya utarajali yataendelea kama ilivyoelezewa na sheria.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari Mchanganyiko

200 wapimwa afya na GGML katika maonesho ya OSHA

Spread the loveZAIDI ya watu 200 jijini Arusha wamejitokeza kupimwa afya na...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

AfyaHabari Mchanganyiko

Songwe katika mikakati ya elimu ya lishe kudhibiti udumavu

Spread the love  SERIKALI mkoani Songwe imejipanga kuendelea kutoa elimu ya lishe...

Afya

Mloganzila yajipanga kupandikizaji wa ini

Spread the love  HOSPITALI ya Taifa Muhimbili-Mloganzila imesema kutokana na uwekezaji uliofanywa...

error: Content is protected !!