Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Ujenzi miradi ya maji washika kasi Musoma Vijijini
Habari Mchanganyiko

Ujenzi miradi ya maji washika kasi Musoma Vijijini

Spread the love

 

UJENZI wa miradi ya maji katika Jimbo la Musoma Vijijini, Mkoa wa Mara, umetajwa kuendelea kushika kasi, ambapo maji kutoka Ziwa Victoria yameanza kusambazwa kwa wananchi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mara … (endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa hivi karibuni na Ofisi ya Mbunge wa Musoma Vijijini, Prof. Sospeter Muhongo, Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA), unaendelea kutekeleza mradi wa maji ya bomba ya Chumwi-Mabuimerafuru.

Taarifa hiyo imesema kuwa, mradi huo unaogharimu fedha kiasi cha Sh. 1.7 bilioni, umepangwa kukamilika kabla ya tarehe 30 Julai mwaka huu.

“Ujenzi unaoendelea kwa wakati huu ni, ujenzi wa tenki lenye ujazo wa lita 300,000 Kijijini Mabuimerafuru. Ujenzi wa vioski vya maji kwenye vijiji vya Chumwi na Mabuimerafuru.Mradi huu una thamani ya Tsh bilioni 1.7 na umepangwa kukamilishwa kabla ya tarehe 30.7.2023. Baadae, sehemu ya pili ya mradi huu ni ya ujenzi wa miundombinu ya kusambaza maji kwenye Vijiji vya Lyasembe na Murangi,” imesema taarifa hiyo.

Mbali na mradi huo, miradi mingine inayotarajiwa kuanza kutekelezwa jimboni humo ni pamoja na kuwasambaza maji ya bomba katika kata za Tegeruka (vijiji vitatu), Mugango (Vijiji vitatu), unaogharimu kiasi cha Sh. 4.75 bilioni.

Taarifa hiyo imesema kuwa, fedha za usambazaji maji hao zipo na kwamba utekelezaji wake utaanza Julai, 2023.

“Maji ya kata hizi mbili yatatoka kwenye bomba la maji la Mugango-Kiabakari-Butiama, ambalo limepangwa kukamilika kabla ya tarehe 30 Juni 2023.Usanifu wa miundombinu ya usambazaji wa maji ya bomba kwenye Kata za Busambara na Kiriba unakaribia kukamilika,” imesema taarifa hiyo na kuongeza.

“Kata hizi 2 zitasambaziwa maji kutoka kwenye tenki la mlima kong lenye ujazo wa lita 500,000. Maji ya tenki hili yatatolewa kwenye Bomba la Maji la Mugango-Kiabakari-Butiama.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga “HIDAYA” chaendelea kuimarika, wananchi wapewa tahadhari

Spread the loveMAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kutoa taarifa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

error: Content is protected !!