TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi za kazi za muda kwa watendaji wa vituo vya uboreshai daftari la kudumu la wapiga kura. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Tangazo la nafasi hizo limetolewa hivi karibuni na tume hiyo.
“Kwa madhumuni ya uboreshai daftari la kudumu la wapiga kura na kwa kuzingatia masharti ya kifungu cha 7(4) cha Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani Na. 1 ya 2024, mkurugenzi wa uchaguzi anakaribisha maombi kutoka kwa watanzania wenye sifa na uwezo wa kujaza nafasi za waandishi na waendeshaji vifaa vya bayometriki,” imesema taarifa hiyo.
Taarifa hiyo imetaja sifa za wanaohitajika, ikiwemo awe mwenye umri wa miaka kuanzia 18 au zaidi, mwenye elimu ya kidato cha nne na ujuzi wa kompyuta na simu janja (Smartphone).
Nashukuru tume ya uchaguzi kwa kutoa nafsi hii kwa vijana. Wengi wao itawasaidia sana.
Mfumo wa waombaji wafanyakazi kwa njia ya mtandao wenye vigezo vyote haupo
Uchaguzi wa aman na haki
Nashkur tume ya uchaguzi kwa kutoa nafasi hizi za ajira kwa vijana itawasaidia sana
Ni vzuri sana
Maombi ya ajira
Naomba pia nami kuajiriwa