Thursday , 9 May 2024
Home Habari Mchanganyiko TMA kutoa tuzo kwa waandishi wa habari
Habari Mchanganyiko

TMA kutoa tuzo kwa waandishi wa habari

Spread the love

MAMLAKA ya Hali ya Hewa nchini Tanzania (TMA), inatarajia kutoa tuzo kwa waandishi wa habari bora wa taarifa za hali ya hewa pamoja na taa

Mkurugenzi TMA, Dk. Agnes Kijazi

rifa za mamlaka hiyo kwa ujumla kwa lengo la kutambua mchango wao katika sayansi ya hali ya hewa nchini. Anaripoti Rhoda Kanuti, Dar es salaam… (endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa umma leo tarehe 14 Aprili 2022 na TMA kupitia Kitengo cha Masoko na Mahusiano, mamlaka hiyo imeandaa tuzo na zawadi hizo kutoa hamasa na kutambua mchango wa waandishi wa habari katika Sayansi ya Hali ya Hewa nchini.

 

“Tumeandaa utaratibu wa kutoa tuzo au zawadi maalum kwa waandishi  wa habari bora  kwa taarifa za hali ya hewa na TMA kwa ujumla” imesema taarifa hiyo.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa waandishi hao, watapatikana kwa uchambuzi wa kina  utakaofanywa na kamati maalum itakayoundwa kupitia habari zote zitakazowasilishwa.

Waandishi wa habari wanatakiwa, kuwasilisha habari zao kupitia njia ya barua pepe ya media @meteo.go.tz.

Pia imesema kazi zitakazoshindanishwa  ni zile zilizoripotiwa kuanzia mwenzi Oktoba mwaka 2021 mpaka mwezi Mei 2022.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoMichezo

Kengold wakabidhiwa kombe NBC Championship

Spread the loveMdhamini mkuu wa Ligi Daraja la Kwanza (NBC Championship) Benki...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia: Matumizi ya nishati safi sio anasa, ladha ipo

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amesema matumizi ya nishati safi kwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC, SILABU waungana kufikisha elimu ya fedha majumbani

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imeingia makubaliano ya ushirikiano...

AfyaHabari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Kisukari cha mimba ni nini?

Spread the loveKisukari cha mimba ni aina ya kisukari kinachotokea kwa baadhi...

error: Content is protected !!