ALIYEKUWA Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi “Sugu”, ametumia maandamano na mkutano wa hadhara wa chama chake cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kufikisha ujumbe kwa mrithi wake, Spika Tulia Ackson. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mbeya … (endelea).
Tukio hilo limetokea leo tarehe 20 Februari 2024, jijini Mbeya baada ya Sugu kutumia mkutano huo kujaribu kuonesha kuwa Spika Tulia ambaye ni Mbunge wa Mbeya Mjini, hakubaliki kwa wapiga kura wake.
Ni baada ya kuwahoji wangapi hawakumchagua Spika Tulia, hawakumjibu lakini alipowauliza wangapi walimchagua katika Uchaguzi Mkuu wa 2020, wengi waliinua mkono na kuitika kwamba walimchagua.
“Hapa mmeonyesha wazi kabisa kwa sababu hizi ni kura, wangapi hawakumchagua Tulia hapa? Wangapi mlimchagua Sugu akaporwa mikono juu. Tutaendelea kuandamana maisha magumu, chakula bei ghali, petrol bei ghali,” amesema Sugu.
Naye Boniface Mwabukusi aliwataka wananchi wa Mbeya Mjini wasimchague Spika Tulia kwa madai kuwa alishiriki kupitisha mkataba wa uwekezaji bandarini aliodai ulikuwa hauna maslahi kwa taifa.
“Kazi yetu moja ya kuwafurahisha watanzania, ni kuhakikisha sio tu kukaribia bungeni bali anapiga picha akiwa kilomita 1,200 akiwa hapa asirudi tena,” alisema Mwabukusi.
Tangu Bunge lipitishe azimio la kubariki mkataba huo, baadhi ya wanasiasa walimvaa Spika Tulia kwa madai kuwa amekubali lipitishe mkataba mbovu. Hata hivyo, kiongozi huyo wa Bunge pamoja na wabunge wake walijitetea kwamba wameupitisha baada ya kujiridhisha hauna shida kisheria.
Leave a comment