SPIKA wa Bunge la Tanzania, Dk. Tulia Ackson amewakumbusha wabunge kuzingatia uvaaji wa mavazi yanayoruhusiwa kikanuni na kuwa tayari kwa jambo lolote ikiwemo kwenda Ikulu kuapishwa kama itatokea hivyo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).
Dk. Tulia ametoa agizo hilo leo Ijumaa, tarehe 11 Februari 2022, bungeni jijini Dodoma akisema, suala hilo huwa halipendwi kuzungumza lakini linakuwa na tija katika uendeshaji sahihi wa shughuli za muhimili huo kwa mujibu wa kanuni walizojiwekea.
“Kanuni zimetuwekea kipimo, lakini kipimo kingine unacho wewe, kabla hujaja humu bungeni wakati unajiandaa wewe jiambie kama umeitwa na Rais kuapishwa umeteuliwa jambo, ndio utoke humo ndani uende Chamwino utakwenda au utaomba kwenda nyumbani kwanza,” amehoji Dk. Tulia
“Hicho ndio kipimo rahisi, ikiwa waziri mkuu kapigiwa simu kwamba mlete fulani nataka kumwapisha kwa nafasi fulani, utamwomba uende kwanza nyumbani au utakwenda moja kwa moja? Kama huwezi kwenda moja kwa moja basi ujue vazi hilo humu ndani haliruhusiwi,” amesema
Leave a comment