Saturday , 25 March 2023
Home Kitengo Michezo Simba yaichapa Jkt, Yaisogelea Yanga
MichezoTangulizi

Simba yaichapa Jkt, Yaisogelea Yanga

Kikosi cha Simba
Spread the love

 

USHINDI wa mabao matatu walioupata Simba dhidi ya JKT Tanzania, ulitosha kuwafanya kuibuka na pointi tatu kwenye mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliofanyika kwenye Uwanja wa Mkapa jijini Dar es Salaam. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea)

Kwa sasa Simba itakuwa inafikisha pointi 45, mara baada ya kucheza michezo 19, nyuma ya Yanga ambao wanaongoza Ligi wakiwa na pointi 49 baada ya kucheza michezo 21.

Mabao ya Simba kwenye mchezo huo yalifungwa na chriss Mugalu kwenye dakika ya  tisa ya mchezo na bao la pili likipachikwa na Luis Miquison dakika ya 38 na kufanya mchezo huo kwenda mapumziko Simba akiongoza kwa mabao 2-0.

Kipindi cha pili kililejea kwa timu zote kushambuliana, huku Jkt wakionesha nia ya kutaka kuchomoa maboa haoyo dakika ya 90+6, John Bocco ambaye aliingia Uwanjani kuchukua nafasi ya Mugalu akapachika bao la tatu na kuifanya Simba kutoka kifua mbele kwenye mchezo huo kwa ushindi wa mabao 3-0.

Mara baada ya matokeo hayo Simba inatarajia kusafiri Siku ya kesho kuelekea nchini Sudan, kwenye mchezo wa michunao ya Ligi ya mabingwa dhidi ya El Merreikh ya Sudan, mchezo wa kundi A, utakaochezwa siku ya ijumaa tarehe 5 Machi 2021.

Simba mpaka sasa ndio vinara kwenye kundi hilo wakiwa na pointi sita mara baada ya kushinda michezo yao miwili ya awali ambapo alifanikiwa kushinda dhidi ya AS Vita ugenini nchini Congo DR na baadae kupata ushindi kwenye mchezo wa pili dhidi ya Al Ahly.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Yanga: Fedha za Rais Samia zinaleta ari kubwa

Spread the loveUONGOZI wa klabu ya Yanga, umesema fedha zinazotolewa na Rais...

Michezo

Simba Sc. yamvulia kofia Rais Samia, yamuahidi makubwa dhidi ya Horoya

Spread the loveWAKATI timu ya Simba ikiibuka na ushindi wa bao 3-0...

Habari MchanganyikoTangulizi

Rais Samia ampandisha cheo RPC wa Dar

Spread the loveMKUU wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Camillus Wambura, amesema...

Habari za SiasaTangulizi

Wanachama 384 CUF watimkia Chadema, Mbowe awapokea, Kambaya ndani…

Spread the loveJUMLA ya wanachama 384 wanachama wa Chama cha Wananchi CUF...

error: Content is protected !!