Wednesday , 6 December 2023
Home Kitengo Maisha Afya Serikali yashusha neema Njombe
Afya

Serikali yashusha neema Njombe

Spread the love

SERIKALI kupitia Wizara ya Afya imeshusha neema kwa wananchi wa Njombe kwa kutenga kiasi cha Sh. 7.6 bilioni kwa ajili ya ujenzi wa awamu ya pili ya ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe ili kuboresha huduma kwa Wananchi. Anaripoti Hamisi Mguta … (endelea). 

Ummy Mwalimu, Waziri wa Afya amezungumza hayo katika zoezi la uzinduzi wa huduma za Afya katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe iliyofunguliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Magufuli.

Katika uzinduzi huo, Waziri Ummy amesema kuwa Serikali inaendelea kuboresha huduma za afya katika Mkoa wa Njombe ikiwemo kujenga jengo la wazazi la ghorofa tatu, jengo la maabara, jengo la wagonjwa mahututi na jengo la upasuaji gorofa mbili, wodi za wagonjwa gorofa tatu, nyumba za Watumishi tano, pamoja na kichomea taka.

“Tunajenga jengo la wazazi la ghorofa tatu, tunajenga jengo la jengo la maabara, tunajenga jengo la wagonjwa mahututi na jengo la upasuaji ghorofa mbili, tunajenga wodi za wagonjwa ghorofa tatu, tunajenga jengo la kufulia, tunajenga kichomea taka na tunajenga nyumba za watumishi tano,” amesema.

Kwa upande mwingine, Waziri Ummy amemwagiza Mkandarasi wa Hospitali hiyo kuhakikisha anakamilisha ujenzi wa majengo hayo hayo ndani ya miezi kumi ili wananchi waanze kufaidika na huduma za Afya katika Hospitali hiyo, huku akiwatoa hofu kuwa pesa zote zipo tayari.

Mbali na hayo, Waziri Ummy amewaasa Wananchi kupambana dhidi ya magonjwa yasiyo yakuambukiza kama kisukari, shinikizo la damu, saratani na magonjwa ya moyo kwa kubadilisha mtindo wa maisha ikiwamo ulaji ulio sahihi, kuacha uvutaji wa sigara na tumbaku, kuacha unywaji wa pombe kupita kiasi pamoja na kutofanya mazoezi mara kwa mara.

Aidha, ametoa wito kwa vijana kujiepusha na mambo ambayo yatapelekea kupata maambukizi ya VVU, huku akiweka wazi kuwa maambukizi mapya ya VVU ni 82,000 kila mwaka nchini Tanzania, huku katika kila watu 100, watu 40 ni vijana wenye umri kati ya 15 hadi 24 umri ambao ni nguvu kazi ya taifa.

“Tunatambua kwamba kuna maambukizi makubwa ya virusi vya Ukimwi Mkoani Njombe, lazima tuzingatie kanuni za kujikinga na maambukizi ya VVU, kujizuia kufanya mapenzi kwa vijana hasa kwa wasichana ambao muda wao haijafika, pili kuwa mwaminifu kwa mwenza wako au mpenzi wako na tatu kutumia kinga,” alisema Waziri Ummy.

Christopher Olesendeka, Mkuu wa mkoa wa Njombe amewatoa hofu wananchi wa mkoa huo kwa kuweka wazi kuwa huduma za Afya katika Hospitali mpya ya Rufaa ya mkoa haitoathiri utoaji huduma katika Hospitali ya Kibena iliyokuwa Hospitali ya Mkoa, ambayo kwa sasa imerudishwa chini ya Halmashauri ya Mji wa Njombe.

“Nitahakikisha wale Watumishi ambao tulikubaliana waje kwenye Hospitali hii, waje na nguo zao, vifaa vyote waviache Kibena na huduma ya Kibena iendelee, na kazi ya Hospitali hii Waziri  na Rais wataweka vifaa vyote vitakavyohitajika na huduma zitaendelea,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari za Siasa

RAS Songwe: Tumepigwa… mkurugenzi nakupa siku 21

Spread the loveKATIBU tawala mkoani Songwe, Happines Seneda ametoa siku 21 kwa...

AfyaHabari Mchanganyiko

Majaliwa aipongeza GGML mapambano dhidi ya Ukimwi

Spread the loveWaziri Mkuu Kassim Majaliwa ameipongeza Kampuni ya Geita Gold Mining...

AfyaHabari Mchanganyiko

GGML waungana na Biteko kuanika mbinu za mapambano dhidi ya Ukimwi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

AfyaMichezo

GGML yatoa milioni 17 kung’arisha ATF Marathon

Spread the loveKATIKA kuendelea kuunga mkono jitihada za Serikali kukabiliana na maambukizi...

error: Content is protected !!