Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Maisha Afya Serikali kujenga madarasa 15,000, vituo vya afya 250
AfyaElimuHabari za Siasa

Serikali kujenga madarasa 15,000, vituo vya afya 250

Spread the love

 

RAIS Samia Suluhu Hassan amesema kuna fedha ambayo ameipata na sasa anatarajia kushirikiana na halmashauri zenye uwezo kifedha kujenga madarasa 15,000 nchi nzima licha ya kuwepo kwa uhaba wa madarsa 11,000 hadi sasa. Anaripoti Noela Shila, TUDARCo … (endelea). 

Pia amesema alipoingia madarakani Machi 19 mwaka huu amekutana tarafa 250 hazina vituo vya afta, hivyo atatumia tozo za miamala ya simu kujenga vituo hivyo katika tarafa zote.

Rais Samia ametoa kauli hiyo leo tarehe 27 Septemba, 2021 jijini Dodoma wakati akihutubia Mkutano Mkuu maalumu wa uchaguzi wa viongozi wakuu wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa (ALAT) wenye kauli mbiu “chagua viongozi bora kwa maendeleo endelevu.”

“Sina maana kwamba halmashauri zenye fedha nyingi hiyo fedha itakuwa exempted kwenye kujenga madarasa hapana.

“Ni ile ambayo serikali kuu itatafuta na halmashauri zenye uwezo tutakwenda kushirikiana kujenga mdarasa hayo 15,000. Lengo ikifika 2022 watoto wote waingie shule kwa pamoja,” amesema.

1 Comment

  • Kuna fedha ambayo ameipata? Kutoka wapi? Ni fedha zake au za umma? Ni tozo na kodi ama mkopo wa IMF? Naomba ufafanuzi

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Afya

Mloganzila yajipanga kupandikizaji wa ini

Spread the love  HOSPITALI ya Taifa Muhimbili-Mloganzila imesema kutokana na uwekezaji uliofanywa...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

error: Content is protected !!