Friday , 29 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Serikali kujenga bandari ya uvuvi Bagamoyo
Habari za Siasa

Serikali kujenga bandari ya uvuvi Bagamoyo

Spread the love

SERIKALI ina mpango wa kujenga bandari ya uvuvi wilayani Bagamoyo, ili kuimarisha shughuli za uchumi wa buluu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Hayo ameyasema Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, leo tarehe 19 Septemba 2023, akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa mradi wa Bandari ya uvuvi unaogharimu Sh. 266 bilioni na ugawaji boti za kisasa kwa wavuvi, Kilwa Masoko mkoani Lindi.

Amesema bandari hiyo itajengwa pale uchumi wa nchi utakaporuhusu, huku akiweka wazi mpango wa Serikali yake ya kuanzisha maeneo ya ufugaji samaki katika ukanda wa pwani ya bahari.

“Kutokana na ukubwa wa ukanda wa Pwani, tunafikiria pia bandari hii niliyoiona na maboto yanavyoletwa na mradi huu, tunataka kuanzisha maeneo ya ufugaji samaki na bandari hii inaweza ikatosha upande huu. Sababu ukanda wetu wa bandari ni mkubwa tunafikiria kujenga bandari nyingine ya uvuvi pale Bagamoyo hali ya uchumi ikituruhusu,” amesema Rais Samia.

Akizungumzia ujenzi wa Bandari ya Uvuvi Kilwa, Rais Samia amesema ukikamilika utasaidia kutoa ajira zaidi ya 20,000 na kutoa fursa mbalimbali ikiwemo za biashara kwa wananchi wa eneo hilo.

Kuhusu boti za kisasa zilizogawiwa kwa wavuvi, Rais Samia amewataka kurejesha kwa wakati mikopo hiyoili nyingine zinunuliwe kwa ajili ya kuwanufaisha wavuvi wengine.

Aidha, Rais Samia amewataka vijana kuchangia fursa za uvuvi ikiwemo kufuga samaki kwa kuwa masoko ya uhakika yapo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Serikali yawaangukia viongozi wa dini

Spread the loveSERIKALI imewaomba viongozi wa dini, waendelee kuelimisha wananchi kudumisha amani...

Habari za Siasa

Azzim Dewji aitaka Serikali iwanyooshe mafisadi

Spread the loveMFANYABIASHARA maarufu nchini, Azzim Dewji, ameitaka Serikali iwachukulie hatua wezi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

Habari za Siasa

Mgongano wa kimasilahi wamhamisha Chande TTCL

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO),...

error: Content is protected !!