Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Selasini ajiuzulu bungeni
Habari za SiasaTangulizi

Selasini ajiuzulu bungeni

Joseph Selasini, Mbunge wa Rombo
Spread the love

JOSEPH Roman Selasini, Mbunge wa Rombo (Chadema), amejiuzulu nafasi ya unadhimu wa Kambi ya Upinzani bungeni. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma…(endelea).

Selasini amechukua hatua hiyo leo tarehe 13 Januari 2020, ambapo ameandikia barua kwenda kwa Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe.

Kwenye barua yake, Selasini amedai, ni kutokana na kutopewa barua rasmi ya kukaimu nafasi hiyo iliyoshikiliwa na Tundu Lissu, Mwanasheria Mkuu wa chama hicho kabla ya kupigwa risasi na kusafiri nje ya nchi kwa ajili ya matibabu.

“Baada ya kutafakari kwa kipindi chote nilichoitumia nafasi hii, hadi sasa ninapoandika barua hii na kwa miaka yote miwili, hujawahi kunipa barua rasmi ya kukaimu nafasi hiyo na kuthibitisha katika utumishi huo.

“Vilevile hujawahi kunipa onyo lolote la mdomo au maandishi kuonyesha kuwa, huridhiki na utendaji wangu,” inaeleza sehemu ya barua hiyo na kuongeza:

“Na kwakuwa ofisi ya Katibu wa Bunge haina uthibitisho wowote wa mdomo au maandishi wa mimi kukaimu nafasi hiyo, ninakutaarifu kwamba, nimejiuzulu nafasi hii kuanzia tarehe ya barua hii.”

Katika barua hiyo ambayo nakala imeelekezwa kwa Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai na Katibu wa Bunge, Steven Kigaigai, Selasini amedai kuwa, amejiuzulu ili ampe nafasi Kiongozi wa Kambi rasmi ya Upinzani Bungeni, kufanya uamuzi wa kumteua mbunge mwingine atakayewaongoza katika kipindi kilichobakia cha uhai wa Bunge hilo.

Aidha, amemshukuru kiongozi huyo wa upinzani kwa imani ya kumteua kukaimu nafasi ya Lissu na kuwa, licha ya kuwasimamia wabunge wenzake, uteuzi wa nafasi hiyo ulimpa fursa ya kuhudhuria na kumuwakilisha katika kamati mbili muhimu bungeni ambazo ni Kamati ya Uongozi na Kamati ya Kanuni.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!