Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Samia: Tumempoteza kiongozi mahiri
Habari za Siasa

Samia: Tumempoteza kiongozi mahiri

Spread the love

RAIS Samia Suluhu Hassan ameeleza kupokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya kifo cha Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Ngoyai Lowassa (70) aliyefariki leo Jumamosi saa nane mchana katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete Jijini (JKCI) Dar es Salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Kupitia akaunti yake ya mtandao wa X (twitter), Rais Samia ameandika; “Lowassa ameitumikia nchi yetu katika nafasi mbalimbali kwa zaidi ya miaka 35, akianzia ushiriki wake katika Jeshi la Wananchi wa Tanzania, Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mbunge, Waziri katika wizara mbalimbali na Waziri Mkuu.

“Tumempoteza kiongozi mahiri, aliyejituma na kujitoa kwa nchi yetu. Natoa pole kwa mjane, Mama Regina Lowassa, watoto (Mheshimiwa Mbunge wa Monduli, Fredrick Lowassa na wadogo zako), ndugu, jamaa, marafiki na Watanzania wote kwa msiba huu mzito.

“Katika mawasiliano yangu na familia, nimewaeleza kuwa kama taifa tuko pamoja nao katika kipindi hiki kigumu, na kamwe wasiache kumtegemea Mwenyezi Mungu na kutafakari neno lake, hasa Kitabu cha Ayubu 1:21. Mwenyezi Mungu amweke mahali pema. Amina,” ameandika Rais Samia.

Kifo cha Lowassa kimetangazwa leo Makamu wa Rais Dk. Philip Mpango kwa niaba ya Rais Samia kupitia televisheni ya Taifa (TBC).

Amesema Lowassa alikuwa akipatiwa matibabu ya ugonjwa wa kujikunja utumbo, matatizo ya mapafu na shinikizo la damu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Biteko aipongeza GGML kudhibiti vifo, majeruhi mahali pa kazi

Spread the loveNAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za Siasa

Askofu Shoo awataka ACT kupigania maslahi ya Taifa, wasikubali kuhongwa

Spread the loveALIYEKUWA Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri, Askofu...

Habari za Siasa

Biteko aagiza waajiri kudhibiti vifo mahali pa kazi

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

error: Content is protected !!