Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Samia: Kamilisheni Sheria kulinda taarifa binafsi za watu
Habari za Siasa

Samia: Kamilisheni Sheria kulinda taarifa binafsi za watu

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

 

RAIS Samia Suluhu Hassan ameielekeza Wizara ya Habari na Teknolojia ya Mawasiliano ya Habari kuhakikisha inakamilsha Sheria ya kulinda taarifa binafsi za watu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Ametoa maelekezo hayo leo Jumatano tarehe 6 Aprili 2022, akizindua mfumo wa usafirishaji wa dharura wa wajawazito na watoto wachanga (M-Mama) jijini Dodoma.

Mkuu huyo wa nchi amesema sheria hiyo itasaidia pia kulinda taarifa za wajawazito zitakazokuwa zinatolewa kwenye mfumo wa M-Mama zisitumike tofauti na ilivyokusudiwa.

“Sio taarifa zimeshakusanywa mama huyo kachukuliwa taarifa zake tumbo lina sentomita ngapi motto yukoje tumboni, taarifa tunazikuta mitandaoni zinasambaa. Hapana.

“Ile Sheria ya kulinda taarifa za watu naomba ikamilishwe na taarifa hizo ziende zikalindwe,” amesema Rais Samia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari za Siasa

Wizara ya Kilimo yapanga kutumia Sh. 1.2 trilioni 2024/25

Spread the loveWIZARA ya Kilimo, imepanga kutumia bajeti ya Sh. 1.2 trilioni...

error: Content is protected !!