Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari Sakata la kina Mdee: Chadema hawajapokea ‘Summons’
HabariHabari za Siasa

Sakata la kina Mdee: Chadema hawajapokea ‘Summons’

Spread the love

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimesema hakijapokea wito wa mahakama kuhusu kesi inayodaiwa kufunguliwa na wanachama wake 19 waliofukuzwa hivi karibuni ndani ya chama hicho. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea)

Kauli hiyo ya Chadema imekuja saa chache baada ya leo tarehe 16 Mei, 2022 Spika wa Bunge, Dk. Tulia Ackson kulitangazia Bunge kuwa ana taarifa kwamba wabunge 19 wa viti maalumu ambao wamefukuzwa uanachama Chadema, wamefungua kesi katika mahakama kuu.

Katika andiko alilolibandika kwenye ukurasa wake wa Twitter, Mkurugenzi wa Mawasiliano, Itifaki na Mambo ya Nje, John Mrema amesema; Kufungua kesi ni jambo moja, kupata amri ya zuio la Mahakamani ni jambo linguine.

“Chadema hatujapewa wito wa Mahakama (Summons) kuhusu kesi hiyo. Spika hajaeleza kupokea amri yoyote ya Mahakama iliyotolewa.

“Hivyo kusema tu kwamba amejulishwa na wahusika kwamba kuna kesi, haitoshi.

Wabunge hao ni Halima Mdee, Grace Tendega, Esther Matiko, Cecilia Pareso, Esther Bulaya, Jesca Kishoa, Hawa Mwaifunga, Tunza Malapo, Naghenjwa Kaboyoka, Sophia Mwakagenda, Kunti Majala, Anatropia Theonest, Salome Makamba na Conchesta Rwamlaza.

Wengine ni Agnesta Kaiza, Nusrat Hanje, Asia Mohamed, Felister Njau na Stela Fiyao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!